Ama kupangusa juu ya viatu, ni jambo limeenea kati ya wanazuoni wa baadaye kuwa haijuzu kupaka juu yake. Nasi hatujui dalili waliyonayo katika hilo isipokuwa yale aliyoyasema al-Bayhaqiy:
”Asili ni wajibu wa kuosha miguu isipokuwa kile kilichothibitishwa na Sunnah thabiti au maafikiano yasiyo na makinzano. Hakuna katika kupaka juu ya viatu wala juu ya soksi mojawapo ya mambo hayo mawili – na Allaah ndiye anayejua zaidi.”[1]
Kwa masikitiko ni kwamba maneno hayo ni kufumbia macho Hadiyth zilizotangulia katika kitabu katika kuthibitisha kupangusa juu ya soksi na viatu. Kwa sababu hiyo at-Turkumaaniy al-Hanafiy alimraddi na akasema:
”Hili halikubaliki. Tayari imeshatangulia kwamba at-Tirmidhiy amesahihisha Hadiyth ya kupaka juu ya soksi na viatu na akaifanya nzuri Hadiyth ya Huzayl kutoka kwa al-Mughiyrah, na pia akaifanya nzuri Hadiyth ya adh-Dhwahhaak kutoka kwa Abu Muusa. Ibn Hibbaan amesahihisha Hadiyth ya Aws kuhusu kupangusa juu ya viatu. Ibn Khuzaymah amesahihisha Hadiyth ya Ibn ´Umar kuhusu kupaka juu ya viatu vya ngozi. Ile Hadiyth ambayo al-Bayhaqiy ameipokea kutoka kwa Zayd bin al-Hubaab, kutoka kwa ath-Thawriy (kutoka kwa Ibn ´Abbaas, kama ilivyotangulia) kuhusu kupaka juu ya viatu ni nzuri. Ibn-ul-Qattwaan ameisahihisha kutoka kwa Ibn ´Umar.”[2]
Ukishayajua haya, basi haijuzu kusita kukubali ruhusa hii baada ya kuthibiti Hadiyth juu yake. Kwa sababu, kama alivyosema mtunzi hapo awali, kwmaba Hadiyth imethibiti na hivyo hakuna isipokuwa kusikia na kutii. Hilo khaswa baada ya kuwa vitendo vya Maswahabah kupita juu ya hilo. Katika kilele chao ni khaliyfah mwongofu ´Aliy bin Abiy Twaalib (Radhiya Allaahu ´anh), kama ilivyotangulia. Isitoshe kitendo hicho kilifanyiwa kazi na wengi katika maimamu wa Salaf (Radhiya Allaahu ´anhum). Ibn Hazm (Rahimahu Allaah) amesema:
”Ikiwa soksi za ngozi zimekatwa chini ya vifundo viwili vya mguu, basi kupaka juu yake kunajuzu. Hayo ndio maoni ya al-Awzaa´iy. Imenukuliwa kutoka kwake kwamba amesema: ”Muhrim apake juu ya soksi mbili zilizokatwa chini ya vifundo.” Wengine wakasema kuwa asipanguse juu yake isipokuwa ziwe juu ya vifundo.”[3]
[1] as-Sunan (1/288).
[2] al-Jawhar an-Naqiy (1/288).
[3] al-Muhallaa (2/103).
- Muhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Itmaam-un-Nush fiy Ahkaam-il-Mash, uk. 82-83
- Imechapishwa: 22/04/2026
Ama kupangusa juu ya viatu, ni jambo limeenea kati ya wanazuoni wa baadaye kuwa haijuzu kupaka juu yake. Nasi hatujui dalili waliyonayo katika hilo isipokuwa yale aliyoyasema al-Bayhaqiy:
”Asili ni wajibu wa kuosha miguu isipokuwa kile kilichothibitishwa na Sunnah thabiti au maafikiano yasiyo na makinzano. Hakuna katika kupaka juu ya viatu wala juu ya soksi mojawapo ya mambo hayo mawili – na Allaah ndiye anayejua zaidi.”[1]
Kwa masikitiko ni kwamba maneno hayo ni kufumbia macho Hadiyth zilizotangulia katika kitabu katika kuthibitisha kupangusa juu ya soksi na viatu. Kwa sababu hiyo at-Turkumaaniy al-Hanafiy alimraddi na akasema:
”Hili halikubaliki. Tayari imeshatangulia kwamba at-Tirmidhiy amesahihisha Hadiyth ya kupaka juu ya soksi na viatu na akaifanya nzuri Hadiyth ya Huzayl kutoka kwa al-Mughiyrah, na pia akaifanya nzuri Hadiyth ya adh-Dhwahhaak kutoka kwa Abu Muusa. Ibn Hibbaan amesahihisha Hadiyth ya Aws kuhusu kupangusa juu ya viatu. Ibn Khuzaymah amesahihisha Hadiyth ya Ibn ´Umar kuhusu kupaka juu ya viatu vya ngozi. Ile Hadiyth ambayo al-Bayhaqiy ameipokea kutoka kwa Zayd bin al-Hubaab, kutoka kwa ath-Thawriy (kutoka kwa Ibn ´Abbaas, kama ilivyotangulia) kuhusu kupaka juu ya viatu ni nzuri. Ibn-ul-Qattwaan ameisahihisha kutoka kwa Ibn ´Umar.”[2]
Ukishayajua haya, basi haijuzu kusita kukubali ruhusa hii baada ya kuthibiti Hadiyth juu yake. Kwa sababu, kama alivyosema mtunzi hapo awali, kwmaba Hadiyth imethibiti na hivyo hakuna isipokuwa kusikia na kutii. Hilo khaswa baada ya kuwa vitendo vya Maswahabah kupita juu ya hilo. Katika kilele chao ni khaliyfah mwongofu ´Aliy bin Abiy Twaalib (Radhiya Allaahu ´anh), kama ilivyotangulia. Isitoshe kitendo hicho kilifanyiwa kazi na wengi katika maimamu wa Salaf (Radhiya Allaahu ´anhum). Ibn Hazm (Rahimahu Allaah) amesema:
”Ikiwa soksi za ngozi zimekatwa chini ya vifundo viwili vya mguu, basi kupaka juu yake kunajuzu. Hayo ndio maoni ya al-Awzaa´iy. Imenukuliwa kutoka kwake kwamba amesema: ”Muhrim apake juu ya soksi mbili zilizokatwa chini ya vifundo.” Wengine wakasema kuwa asipanguse juu yake isipokuwa ziwe juu ya vifundo.”[3]
[1] as-Sunan (1/288).
[2] al-Jawhar an-Naqiy (1/288).
[3] al-Muhallaa (2/103).
Muhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Itmaam-un-Nush fiy Ahkaam-il-Mash, uk. 82-83
Imechapishwa: 22/04/2026
https://firqatunnajia.com/02-kupangusa-juu-ya-viatu/