Swali 2: Kijana ambaye anaweza kuyapambanua mambo aamrishwe kufunga? Je, itasihi kwake iwapo atabaleghe katikati ya mchana?
Jibu: Kumetangulia katika jibu la swali la kwanza ya kwamba mtoto wa kiume na wa kike wakifikisha miaka saba na zaidi basi wanatakiwa kuamrishwa kufunga ili waizowee. Ni lazima kwa wasimamizi wao kuwaamrisha kama wanavyowaamrisha kuswali. Wakishabaleghe basi watalazimika kufunga. Wakibaleghe katikati ya mchana basi siku hiyo itasihi kwao. Tukadirie kuwa mvulana amefikisha miaka kumi na tano wakati wa kupindukia kwa jua ilihali amefunga basi siku hiyo itasihi kwake. Sehemu ya mwanzo ya mchana itakuwa ni Sunnah kwake na sehemu ya mwisho ya mchana itakuwa ni faradhi. Hapo ni pale ambapo alikuwa hakubaleghe kabla ya hapo kwa kuota nywele kwenye makwapa au kutokwa na manii kwa matamanio. Vilevile inahusiana na mtoto wa kike. Wawili hao wana hukumu moja. Pamoja na kwamba kuna jambo la nne linalozidi kwa mtoto wa kike ambalo hubaleghe kwalo. Nalo ni kupata hedhi.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdllaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: As-ilah Muhimmah tata´alaqah bisw-Swiyaam, uk. 05
- Imechapishwa: 02/04/2019
Swali 2: Kijana ambaye anaweza kuyapambanua mambo aamrishwe kufunga? Je, itasihi kwake iwapo atabaleghe katikati ya mchana?
Jibu: Kumetangulia katika jibu la swali la kwanza ya kwamba mtoto wa kiume na wa kike wakifikisha miaka saba na zaidi basi wanatakiwa kuamrishwa kufunga ili waizowee. Ni lazima kwa wasimamizi wao kuwaamrisha kama wanavyowaamrisha kuswali. Wakishabaleghe basi watalazimika kufunga. Wakibaleghe katikati ya mchana basi siku hiyo itasihi kwao. Tukadirie kuwa mvulana amefikisha miaka kumi na tano wakati wa kupindukia kwa jua ilihali amefunga basi siku hiyo itasihi kwake. Sehemu ya mwanzo ya mchana itakuwa ni Sunnah kwake na sehemu ya mwisho ya mchana itakuwa ni faradhi. Hapo ni pale ambapo alikuwa hakubaleghe kabla ya hapo kwa kuota nywele kwenye makwapa au kutokwa na manii kwa matamanio. Vilevile inahusiana na mtoto wa kike. Wawili hao wana hukumu moja. Pamoja na kwamba kuna jambo la nne linalozidi kwa mtoto wa kike ambalo hubaleghe kwalo. Nalo ni kupata hedhi.
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdllaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: As-ilah Muhimmah tata´alaqah bisw-Swiyaam, uk. 05
Imechapishwa: 02/04/2019
https://firqatunnajia.com/02-kijana-ambaye-anaweza-kuyapambanua-mambo-aamrishwe-kufunga/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)