120- Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) ameeleza kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Yule mwenye kuulizwa juu ya elimu akaificha, basi atapigwa hatamu ya Moto siku ya Qiyaamah.”[1]
Ameipokea Abu Daawuud, at-Tirmidhiy aliyesema kuwa ni nzuri, Ibn Maajah, Ibn Hibbaan katika ”as-Swahiyh”, al-Bayhaqiy na al-Haakim amepokea mfano wake na akasema:
“Swahiyh juu ya sharti za al-Bukhaariy na Muslim. Lakini hawakuitoa.”
Katika upokezi wa Ibn Maajah imekuja:
“Hakuna mtu yeyote atakayehifadhi elimu kisha akaificha isipokuwa atalaletwa siku ya Qiyaamah amepigwa kwa hatamu ya Moto.”[2]
[1] Swahiyh.
[2] Swahiyh kupitia zengine.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Adhwiym bin ´Abdil-Qawiy al-Mundhiriy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Swahiyh-ut-Targhiyb wat-Tarhiyb (1/160)
- Imechapishwa: 03/05/2020
- Taaliki: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)