Swali: Baba yangu hafungi. Je, nimtolee Zakaat-ul-Fitwr?

Jibu: Kama anaacha kufunga kwa kukusudia kwa sababu anaona kuwa sio wajibu, ni kafiri. Ama kama anaacha kufunga kwa sababu ya uvivu hakufuru. Hata hivyo mtawala amlazimishe kufunga pamoja na wewe kumuaidhi na kumnasihi. Hata hivyo sio kafiri na hivyo ni lazima kwake kutoa zakaah.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (17) https://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/umdtf-08011435.mp3
  • Imechapishwa: 20/10/2019