Wanaosikiliza darsa za live wanaingia katika Hadiyth hii?

Swali: Sisi hivi sasa tunakupata vizuri na tuko Buraydah. Je, tunapata thawabu na tunaingia katika Hadiyth ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) isemayo:

“Hawakusanyiki watu katika nyumba miongoni mwa nyumba za Allaah, wakikisoma Kitabu cha Allaah na wakadarasishana baina yao, isipokuwa huteremka juu yao utulivu, rehema huwafunika, Malaika huwazunguka na Allaah huwataja kwa wale walioko pamoja Naye.”[1]

Jibu: Ndio, natarajia hivo. Kwa sababu kukusanyika kwenu na huku mnasikiliza kupitia spika ni kama watu wanavyokusanyika kwenye kipaza sauti. Nyinyi hivi sasa mnasikiliza kupitia simu kama ambavyo watu wanasikiliza kwenye kipaza sauti. Nyinyi – Allaah akitaka – tunatarajia kwenu ujira na thawabu.

[1] Ameipokea Muslim (2699).

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Liqaa´ ash-Shahriy (73) http://binothaimeen.net/content/1711
  • Imechapishwa: 19/04/2020