Swali: Ambaye atadhihirisha na kufanya mambo yasiyokuwa ya kawaida mbele ya umati tuhukumu kuwa ni katika mawalii wa Allaah? Je, inajuzu kwetu kuomba ponyo kutoka kwake kwa idhini ya Allaah?
Jibu: Kuhukumu kuwa ni walii wa Allaah kwa sababu tu amefanya jambo lisilokuwa la kawaida si sahihi. Ni lazima kwanza kutazama matendo yake. Ni kweli kwamba itakuwa ni karama iwapo matendo yake ni mema na ´Aqiydah yake ni sahihi.
Lakini walii wa kihakika hadhihirishi mambo haya mbele ya watu. Badala yake humnyenyekea Allaah. Walii wa kihakika haingiwi na kiburi na kujiona kwa sababu ya karama hizi. Kinyume chake hujitahidi huzificha kadri na anavyoweza na hazidhihirishi mbele ya watu. Endapo atafanya hivo huashiriwa kidole. Lakini kwa hali yoyote tazama matendo yake na yale anayofuata. Katika hali hiyo ima atakuwa ni walii wa Allaah kweli na hivyo [ayafanyayo] itakuwa ni karama au akawa ni adui wa Allaah na hivyo [ayafanyayo] itakuwa ni mambo ya kishaytwaan.
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Furqaan (01) http://alfawzan.af.org.sa/node/2044
- Imechapishwa: 06/10/2016
Swali: Ambaye atadhihirisha na kufanya mambo yasiyokuwa ya kawaida mbele ya umati tuhukumu kuwa ni katika mawalii wa Allaah? Je, inajuzu kwetu kuomba ponyo kutoka kwake kwa idhini ya Allaah?
Jibu: Kuhukumu kuwa ni walii wa Allaah kwa sababu tu amefanya jambo lisilokuwa la kawaida si sahihi. Ni lazima kwanza kutazama matendo yake. Ni kweli kwamba itakuwa ni karama iwapo matendo yake ni mema na ´Aqiydah yake ni sahihi.
Lakini walii wa kihakika hadhihirishi mambo haya mbele ya watu. Badala yake humnyenyekea Allaah. Walii wa kihakika haingiwi na kiburi na kujiona kwa sababu ya karama hizi. Kinyume chake hujitahidi huzificha kadri na anavyoweza na hazidhihirishi mbele ya watu. Endapo atafanya hivo huashiriwa kidole. Lakini kwa hali yoyote tazama matendo yake na yale anayofuata. Katika hali hiyo ima atakuwa ni walii wa Allaah kweli na hivyo [ayafanyayo] itakuwa ni karama au akawa ni adui wa Allaah na hivyo [ayafanyayo] itakuwa ni mambo ya kishaytwaan.
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Furqaan (01) http://alfawzan.af.org.sa/node/2044
Imechapishwa: 06/10/2016
https://firqatunnajia.com/walii-wa-kweli-hafanyi-haya-mbele-za-watu/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)