Swali 16: Baadhi ya watu wanamkaripia yule anayeswali bila ya kilemba. Ni ipi dalili inayokataza? Je, kuvaa kilemba ni Sunnah au hapana?
Jibu: Kilemba kinazingatiwa ni miongoni mwa zile ada za waarabu ambazo zilikubaliwa na Uislamu. Kusema kwamba kilemba kinafikia kiwango cha Sunnah hakifikii kiwango cha Sunnah. Kinazingatiwa ni ada. Lakini mtu akinuia kumuigiliza Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) basi analipwa thawabu kwa kumuigiliza Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
Ama kuswali pasi na kilemba ni sahihi. Haitakikani kumkemea mtu anayeswali pasi na kilemba. Haifai kumkemea yeyote isipokuwa kwa dalili kutoka katika Qur-aan na Sunnah. Tunachowanasihi watu ni kuvaa kilemba ndani ya swalah na nje ya swalah. Lakini iwapo atatoka mtu kichwa chake kikiwa wazi asikaripiwe. Hatusemi kuwa swalah yake ni batili.
- Mhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Tuhfat-ul-Mujiyb, uk. 138
- Imechapishwa: 24/12/2019
Swali 16: Baadhi ya watu wanamkaripia yule anayeswali bila ya kilemba. Ni ipi dalili inayokataza? Je, kuvaa kilemba ni Sunnah au hapana?
Jibu: Kilemba kinazingatiwa ni miongoni mwa zile ada za waarabu ambazo zilikubaliwa na Uislamu. Kusema kwamba kilemba kinafikia kiwango cha Sunnah hakifikii kiwango cha Sunnah. Kinazingatiwa ni ada. Lakini mtu akinuia kumuigiliza Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) basi analipwa thawabu kwa kumuigiliza Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).
Ama kuswali pasi na kilemba ni sahihi. Haitakikani kumkemea mtu anayeswali pasi na kilemba. Haifai kumkemea yeyote isipokuwa kwa dalili kutoka katika Qur-aan na Sunnah. Tunachowanasihi watu ni kuvaa kilemba ndani ya swalah na nje ya swalah. Lakini iwapo atatoka mtu kichwa chake kikiwa wazi asikaripiwe. Hatusemi kuwa swalah yake ni batili.
Mhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Tuhfat-ul-Mujiyb, uk. 138
Imechapishwa: 24/12/2019
https://firqatunnajia.com/swalah-na-kilemba/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)