Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“… Swadaqah inazima madhambi kama vile maji yanavyozima moto.”
swadaqah kwa aina zake mbali mbali inafuta madhambi. Haijalishi kitu sawa ikiwa ni swadaqah kwa maneno, matendo ya wajibu na yaliyopendekezwa. Vilevile swadaqah ya mali. Zote hizi zinafuta madhambi kwa kuwa ni matendo mema. Allaah (Jalla wa ´Aaa) Amesema:
إِنَّ الْحَسَنَاتِ يُذْهِبْنَ السَّيِّئَاتِ
“Hakika mema yanaondosha maovu.” (11:114)
Isitoshe tumebainisha maana ya maneno ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Mche Allaah popote pale ulipo, fuatisha kitendo kiovu kwa kitendo kizuri kitafuta [kitendo kiovu] na ishi na watu kwa uzuri.”
Ukifahamu maana ya swadaqah ya jumla, basi kila pale ambapo utapitikiwa na dhambi, basi ni juu yake kutoa swadaqah sana. Madhambi hayahesabiki. Kwa kuwa hakuna hali yoyote ile utayokuwemo, isipokuwa Allaah ima amekuamrisha au amekukataza [jambo] katika hali hiyo. Ni wachache wenye kutekeleza maamrisho na makatazo katika hali zote. Kwa hivyo, ni lazima mtu kukithirisha kutoa swadaqah kwa wingi. Swadaqah ni milango ya kheri.
- Mhusika: Shaykh Swaalih bin ´Abdil-´Aziyz Aalush-Shaykh
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh al-Arba´iyn an-Nawawiyyah, uk. 407
- Imechapishwa: 14/05/2020
Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“… Swadaqah inazima madhambi kama vile maji yanavyozima moto.”
swadaqah kwa aina zake mbali mbali inafuta madhambi. Haijalishi kitu sawa ikiwa ni swadaqah kwa maneno, matendo ya wajibu na yaliyopendekezwa. Vilevile swadaqah ya mali. Zote hizi zinafuta madhambi kwa kuwa ni matendo mema. Allaah (Jalla wa ´Aaa) Amesema:
إِنَّ الْحَسَنَاتِ يُذْهِبْنَ السَّيِّئَاتِ
“Hakika mema yanaondosha maovu.” (11:114)
Isitoshe tumebainisha maana ya maneno ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Mche Allaah popote pale ulipo, fuatisha kitendo kiovu kwa kitendo kizuri kitafuta [kitendo kiovu] na ishi na watu kwa uzuri.”
Ukifahamu maana ya swadaqah ya jumla, basi kila pale ambapo utapitikiwa na dhambi, basi ni juu yake kutoa swadaqah sana. Madhambi hayahesabiki. Kwa kuwa hakuna hali yoyote ile utayokuwemo, isipokuwa Allaah ima amekuamrisha au amekukataza [jambo] katika hali hiyo. Ni wachache wenye kutekeleza maamrisho na makatazo katika hali zote. Kwa hivyo, ni lazima mtu kukithirisha kutoa swadaqah kwa wingi. Swadaqah ni milango ya kheri.
Mhusika: Shaykh Swaalih bin ´Abdil-´Aziyz Aalush-Shaykh
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh al-Arba´iyn an-Nawawiyyah, uk. 407
Imechapishwa: 14/05/2020
https://firqatunnajia.com/swadaqah-inafuta-madhambi/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)