Inatakikana kwa mtu asiyekuwa asiyejishughulisha na mambo ya elimu kutomuuliza Muftiy dalili. Wala haifai kwake kusema: “Kwa nini umesema.. ?”

Kama atapenda kuituliza nafsi yake kwa kusikiliza dalili, basi aitafute [kutoka kwa mwanachuoni huyo] katika kikao kingine au katika kikao hichohicho lakini baada ya kuwa ameshakubali hiyo fatwah kavu.

  • Mhusika: Imaam Yahyaa bin Sharaf an-Nawawiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Aadaab-ul-Fatwaa, uk. 85
  • Imechapishwa: 29/12/2019