Ni nani anayestahiki kuwa imamu katika hali hii?

Swali: Mtu akiingia baada ya kuwa ameshapitwa na swalah ya Maghrib ambapo akasimama mtu na kutaka kumpa swadaqah. Ni yupi ana haki zaidi ya kuswali na mwingine? Je, kuna ubaya wa kuirudi swalah ya Maghrib ambayo ni Witr ya mchana?

Jibu: Akiingia mtu msikitini na akataka mtu mwingine kumtolea swadaqah, yule mwenye kuonelea kuwa ambaye anaswali swalah ya Sunnah hasihi kuwa imamu wa anayeswali swalah ya faradhi basi itatakikana kwa yule aliyeingia ndiye awe imamu. Kwa sababu mtu huyu anaswali faradhi na huyu wa pili anaswali Sunnah. Upande mwingine yule mwenye kuonelea kuwa inafaa kwa ambaye anaswali swalah ya Sunnah kuwa imamu wa anayeswali swalah ya faradhi – na haya ndio maoni sahihi – wamesema kuwa ataongoza swalah yule ambaye ni msomi zaidi wa Qur-aan. Ni mamoja yule aliyeingia au yule ambaye tayari yuko msikitini.

Kuhusu swali lake juu ya swalah ya Maghrib kwamba irudiwe au isirudiwe, tunaona kuwa irudiwe. Itakuwa Witr kabisa kama swalah ya imamu. Haipingani ile swalah ya kwanza aliyoswali na imamu wa kwanza ndio ikawa Witr ya mchana na hii ya pili ikawa ni marudilio. Hakuna ubaya wake akairudi mara tatu kwa sababu ameirudi akimfuata imamu wake.

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (47) http://binothaimeen.net/content/1086
  • Imechapishwa: 30/03/2019