Jahmiyyah, Mu´tazilah na Haruuriyyah wamesema maneno ya Allaah (´Azza wa Jall):
الرَّحْمَـٰنُ عَلَى الْعَرْشِ اسْتَوَىٰ
“Mwingi wa huruma amelingana juu ya ´Arshi.”[1]
maana yake kwamba Amelingana na ameimiliki na kwamba Allaah (´Azza wa Jall) yuko kila mahali. Wanapinga Allaah (´Azza wa Jall) kuwa juu ya ´Arshi, kama wanavyosema Ahl-ul-Haqq. Wanaonelea kuwa kulingana ni kuweza.
Mambo yangelikuwa hivo wanavyosema basi kusingelikuwa tofauti yoyote kati ya ´Arshi na ardhi ya saba, kwa kuwa ana Allaah umiliki juu ya kila kitu.
Endapo kulingana kwa Allaah juu ya ´Arshi maana yake ingelikuwa ni kutawala – kwani Yeye si ana utawala juu ya kila kitu – basi kulingana Kwake kungelikuwa juu ya ´Arshi, mbingu, ardhi, mashamba ya mitende, takataka na watu, kwa kuwa ana utawala juu ya kila kitu. Ikiwa Allaah ana utawala juu ya kitu, basi haijuzu kwa muislamu yeyote yule kusema kuwa Allaah (´Azza wa Jall) amelingana juu ya mashamba ya mitende na vyoo. Ametakasika Allaah kutokamana na kitu kama hicho. Kwa hiyo ingelikuwa haijuzu kutofautisha ´Arshi na kulingana kwa kuwa Allaah ana utawala juu ya kila kitu. Kwa ajili hiyo kulingana ni maalum na ´Arshi na si chengine.
[1] 20:05
- Mhusika: Imaam Abul-Hasan ´Aliy bin Ismaa´iyl al-Ash´ariy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Ibaanah, uk. 34
- Imechapishwa: 14/04/2017
Jahmiyyah, Mu´tazilah na Haruuriyyah wamesema maneno ya Allaah (´Azza wa Jall):
الرَّحْمَـٰنُ عَلَى الْعَرْشِ اسْتَوَىٰ
“Mwingi wa huruma amelingana juu ya ´Arshi.”[1]
maana yake kwamba Amelingana na ameimiliki na kwamba Allaah (´Azza wa Jall) yuko kila mahali. Wanapinga Allaah (´Azza wa Jall) kuwa juu ya ´Arshi, kama wanavyosema Ahl-ul-Haqq. Wanaonelea kuwa kulingana ni kuweza.
Mambo yangelikuwa hivo wanavyosema basi kusingelikuwa tofauti yoyote kati ya ´Arshi na ardhi ya saba, kwa kuwa ana Allaah umiliki juu ya kila kitu.
Endapo kulingana kwa Allaah juu ya ´Arshi maana yake ingelikuwa ni kutawala – kwani Yeye si ana utawala juu ya kila kitu – basi kulingana Kwake kungelikuwa juu ya ´Arshi, mbingu, ardhi, mashamba ya mitende, takataka na watu, kwa kuwa ana utawala juu ya kila kitu. Ikiwa Allaah ana utawala juu ya kitu, basi haijuzu kwa muislamu yeyote yule kusema kuwa Allaah (´Azza wa Jall) amelingana juu ya mashamba ya mitende na vyoo. Ametakasika Allaah kutokamana na kitu kama hicho. Kwa hiyo ingelikuwa haijuzu kutofautisha ´Arshi na kulingana kwa kuwa Allaah ana utawala juu ya kila kitu. Kwa ajili hiyo kulingana ni maalum na ´Arshi na si chengine.
[1] 20:05
Mhusika: Imaam Abul-Hasan ´Aliy bin Ismaa´iyl al-Ash´ariy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Ibaanah, uk. 34
Imechapishwa: 14/04/2017
https://firqatunnajia.com/ndio-maana-kulingana-kwa-allaah-ni-kitu-maalum-juu-ya-arshi/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)