Mzee mgonjwa hawezi kutawadha kwa maji badala yake anatayamamu

Swali: Muulizaji anasema kuwa mzazi wake kafikisha zaidi ya miaka 85 naye ni mgonjwa hawezi kutia Wudhuu kwa maji. Tunampa udongo atayamamu kwao. Je, inajuzu kwake kutayamamu kwa udongo huu mwezi au zaidi?

Jibu: Ndio, hakuna neno. Atatumia udongo mpaka katika muda maalumu. Maadamu anapata udongo, Alhamdulillaah.

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaa Nuur ´alaad-Darb (770)
  • Imechapishwa: 16/03/2018