Swali: Kuna mwanafunzi ambaye ana dhamira ya kusoma kwelikweli na anataka mwongozo na nuru. Je, unampendekeza kuhifadhi kwanza au kuelewa? Ni mutuni zipi unazopendekeza ahifadhi?
Jibu: Mimi nampendekeza ahifadhi kwanza yule ambaye bado ni mdogo. Kwa sababu mdogo anatofautiana na mkubwa inapokuja katika kuhifadhi kwa mambo mawili:
1- Uharaka wa kuhifadhi.
2- Kutosahau.
Kwa ajili hiyo kuna mithali ambayo ni maarufu isemayo:
“Elimu utotoni ni kama kuchonga kwenye jiwe.”
Jengine ni kwamba akili ya mtoto haiwezi kubeba kufafanuliwa maana na kumtilia uzito kwa sababu bado ni mdogo. Hili ni mosi.
Pili: Kitu cha kwanza na ambacho ni bora zaidi kinachotakiwa kuhifadhiwa ni Kitabu cha Allaah (´Azza wa Jall). Hili ndio jambo la kwanza. Kwa sababu ukihifadhi Qur-aan ndio msingi katika kuthibitisha hukumu na dalili. Ukikihifadhi na unaweza kukisoma katika hali zote – midhali huna janaba – unaweza kukisoma na huku watembea, ndani ya gari, unaweza kukisoma ukiwa juu ya kitanda chako na katika nyakati zengine midhali huna janaba au sehemu ambazo hazistahiki Qur-aan kusomwa nafasi hiyo.
Kisha baada ya hapo yale yaliyosihi kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na khaswa khaswa vile vitabu vilivyokhusisha hilo kama “´Umdat-ul-Ahkaam”. Yaliyomo ndani yametolewa katika “as-Swahiyh” mbili. Halafu yale waliyoandika wanachuoni katika Fiqh. Bora katika yale tunayoona sisi ni “Zaad-ul-Mustaqniy´ fiy Ikhtiswaar-il-Muqniy´”. Mwalimu wetu Shaykh ´Abdur-Rahmaan bin Sa´diy (Rahimahu Allaah) alikuwa akitupendezea nacho na akisema kwamba ni katika vitabu vilivyokusanya na vifupi. Jengine ni kwa kuwa wanachuoni wamekifafanua kwa wingi, kuweka maelezo ya chini, taaliki na mengineyo.
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (38) http://binothaimeen.net/content/856
- Imechapishwa: 19/06/2018
Swali: Kuna mwanafunzi ambaye ana dhamira ya kusoma kwelikweli na anataka mwongozo na nuru. Je, unampendekeza kuhifadhi kwanza au kuelewa? Ni mutuni zipi unazopendekeza ahifadhi?
Jibu: Mimi nampendekeza ahifadhi kwanza yule ambaye bado ni mdogo. Kwa sababu mdogo anatofautiana na mkubwa inapokuja katika kuhifadhi kwa mambo mawili:
1- Uharaka wa kuhifadhi.
2- Kutosahau.
Kwa ajili hiyo kuna mithali ambayo ni maarufu isemayo:
“Elimu utotoni ni kama kuchonga kwenye jiwe.”
Jengine ni kwamba akili ya mtoto haiwezi kubeba kufafanuliwa maana na kumtilia uzito kwa sababu bado ni mdogo. Hili ni mosi.
Pili: Kitu cha kwanza na ambacho ni bora zaidi kinachotakiwa kuhifadhiwa ni Kitabu cha Allaah (´Azza wa Jall). Hili ndio jambo la kwanza. Kwa sababu ukihifadhi Qur-aan ndio msingi katika kuthibitisha hukumu na dalili. Ukikihifadhi na unaweza kukisoma katika hali zote – midhali huna janaba – unaweza kukisoma na huku watembea, ndani ya gari, unaweza kukisoma ukiwa juu ya kitanda chako na katika nyakati zengine midhali huna janaba au sehemu ambazo hazistahiki Qur-aan kusomwa nafasi hiyo.
Kisha baada ya hapo yale yaliyosihi kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na khaswa khaswa vile vitabu vilivyokhusisha hilo kama “´Umdat-ul-Ahkaam”. Yaliyomo ndani yametolewa katika “as-Swahiyh” mbili. Halafu yale waliyoandika wanachuoni katika Fiqh. Bora katika yale tunayoona sisi ni “Zaad-ul-Mustaqniy´ fiy Ikhtiswaar-il-Muqniy´”. Mwalimu wetu Shaykh ´Abdur-Rahmaan bin Sa´diy (Rahimahu Allaah) alikuwa akitupendezea nacho na akisema kwamba ni katika vitabu vilivyokusanya na vifupi. Jengine ni kwa kuwa wanachuoni wamekifafanua kwa wingi, kuweka maelezo ya chini, taaliki na mengineyo.
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (38) http://binothaimeen.net/content/856
Imechapishwa: 19/06/2018
https://firqatunnajia.com/mwanafunzi-aanze-kuhifadhi-au-kuelewa-kwanza/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)