Muweza ameswali kwa kukaa kabla ya Rukuu´

Swali: Baadhi ya watu wanaoweza kusimama wanakaa katika Rak´ah ya pili ya Fajr mpaka pale imamu anapokaribia kwenda katika Rukuu´ hapo ndipo wanasimama na kurukuu pamoja naye. Je, swalah zao sahihi?

Jibu: Hapana. Ameacha nguzo ambayo ni ya kusimama. Ni lazima asimame kabla ya Rukuu´ chinichini kwa kiasi angalau cha kusoma al-Faatihah. Akisimama chini ya hapo pasi na udhuru, basi swalah yake si sahihi, kwa sababu ameacha nguzo. Zindukeni juu ya hili.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (14) https://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/Umdah-03-11-1434.mp3
  • Imechapishwa: 04/05/2019