Swali: Imamu akiswali Tarawiyh Rak´ah tatu kwa kujengea kwamba alikuwa anakusudia kuswali Rak´ah mbili. Je, katika Sunnah kumetajwa kwamba atasujudu sijda ya kusahau?
Jibu: Ndio, ipo sijda ya kusahau ikiwa alikuwa amekusudia kuswali Rak´ah mbili kawaida. Kwa sababu Sunnah juu ya swalah ya usiku ni Rak´ah mbilimbili. Akisimama katika Rak´ah ya tatu anatakiwa kuzindushwa kwa kuambiwa:
سبحان الله
“Allaah ametakasika kutokamana na mapungufu.”
Katika hali hiyo atatakiwa kurudi na kukamilisha Tahiyyaat, kumswalia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kuomba du´aa. Kisha asujudu sijda ya kusahau na kisha atoe salamu. Akipitiliza na asiketi chini atatakiwa kuzinduliwa mpaka aketi chini hata kama ni baada ya Rak´ah ya tatu. Anatakiwa kuketi chini, asome Tahiyyaat na yanayokuja baada yake katika kumswalia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kuomba du´aa. Halafu asujudu sijda ya kusahau na kutoa salamu. Kama ambavo sijda ya kusahau imesuniwa katika swalah ya faradhi vivyo hivyo imesuniwa katika swalah ya sunnah.
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (16/30)
- Imechapishwa: 06/05/2020
Swali: Imamu akiswali Tarawiyh Rak´ah tatu kwa kujengea kwamba alikuwa anakusudia kuswali Rak´ah mbili. Je, katika Sunnah kumetajwa kwamba atasujudu sijda ya kusahau?
Jibu: Ndio, ipo sijda ya kusahau ikiwa alikuwa amekusudia kuswali Rak´ah mbili kawaida. Kwa sababu Sunnah juu ya swalah ya usiku ni Rak´ah mbilimbili. Akisimama katika Rak´ah ya tatu anatakiwa kuzindushwa kwa kuambiwa:
سبحان الله
“Allaah ametakasika kutokamana na mapungufu.”
Katika hali hiyo atatakiwa kurudi na kukamilisha Tahiyyaat, kumswalia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kuomba du´aa. Kisha asujudu sijda ya kusahau na kisha atoe salamu. Akipitiliza na asiketi chini atatakiwa kuzinduliwa mpaka aketi chini hata kama ni baada ya Rak´ah ya tatu. Anatakiwa kuketi chini, asome Tahiyyaat na yanayokuja baada yake katika kumswalia Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kuomba du´aa. Halafu asujudu sijda ya kusahau na kutoa salamu. Kama ambavo sijda ya kusahau imesuniwa katika swalah ya faradhi vivyo hivyo imesuniwa katika swalah ya sunnah.
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (16/30)
Imechapishwa: 06/05/2020
https://firqatunnajia.com/mswaliji-amesahau-akasimama-rakah-ya-tatu-katika-tarawiyh/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)