Tunawanasihi ndugu zetu wa Indonesia walinganie katika dini ya Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala), wafanye ´amali zao kwa kumtakasia Allaah (´Azza wa Jall), watilie umuhimu mkubwa katika kusoma na kufundisha na kulingania katika dini ya Allaah. Pesa ambazo jumuiya ya Ihyaa´ at-Turaath inachangia zitakuja kupotea. Wanaenda kwa wafanya biashara na kusema tuna vyuo, taasisi, watoto mayatima na hili na lile. Matunda yako wapi?

Ihyaa´ at-Turaath iko kwa muda ambao si mdogo. Da´wah ya ´Abdur-Rahmaan ´Abdul-Khaaliq ipo tangu sisi tungali al-Madiynah, zaidi ya miaka 26 au 27. Matunda yako wapi? Ninampa changamoto ´Abdur-Rahmaan ´Abdul-Khaaliq kunilitea mwanafunzi mmoja katika wanafunzi zake ambaye amesoma kwake tu na ana elimu iliobobea. Kadhalika ninawapa changamoto Suruuriyyah ambaye amesoma tu kwa Muhammad Suruur na ana elimu iliobobea. Allaah bado Ataendelea kuwalipiza maadamu wanawavamia Ahl-us-Sunnah.

  • Mhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://muqbel.net/sounds.php?sound_id=21
  • Imechapishwa: 14/07/2020