Mashaytwaan Wanaweza Kuwasaidia Makafiri Vita?

Swali: Je, mashaytwaan wanapigana vita bega kwa bega pamoja na makafiri?

Jibu: Kuhusu mashaytwaan kupigana vita bega kwa bega pamoja na makafiri sijui. Halikuthibiti hili. Bali wanawaghuri makafiri kisha wanawakimbia. Kwa kuwa ni maadui wa mwanaadamu. Vipi watawanusuru ilihali ni maadui wao? Haikuthibiti kuwa mashaytwaan wanapigana vita bega kwa bega pamoja na makafiri. Ni waoga zaidi kuliko hivo. Wanamhadaa mwanaadamu kisha wanamkimbia.

Swali: Je, Malaika wanaweza kuteremka hii leo kuwanusuru waumini?

Jibu: Tumetangulia kusema haya ya kwamba Allaah anawatia nguvu waumini kwa Malaika. Lakini sio kama wanavyowatia nguvu Mitume.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Furqaan (15) http://alfawzan.af.org.sa/node/2058
  • Imechapishwa: 28/04/2017