Swali: Hii leo kuna makubadhi yanayofanana kama khofu. Isipokuwa tu vyenyewe vinaenda mpaka chini ya kongo mbili za miguu na vinafunika eneo lote la chini ya mguu. Makubadhi haya yanafaa wakati wa Ihraam?

Jibu: Ndio, hakuna neno. Kilichokatazwa ni kufunika vifundo vya miguu. Isipokuwa akikosa viatu basi avivae hata kama vinafunika vifundo vya miguu kwa sababu ya haja.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (21) https://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/Umdah-13-2-1435-01.mp3
  • Imechapishwa: 22/02/2020