Lililo salama zaidi kwa mtu atawadhe baada ya kuoga janaba

Swali: Kuoga janaba kwa njia inayotosheleza kunaangusha uwajibu wa kutia wudhuu´[1]?

Jibu: Wanachuoni wametofautiana juu ya hilo. Wako wanachuoni waliosema kwamba mtu akijisafisha tupu yake vizuri kwa maji kisha akaeneza maji vizuri hadathi inaondoka. Wapo wengine waliosema kwamba ni lazima kwa mtu kutawadha. Lililo salama zaidi kwa mtu atawadhe.

[1] Tazama https://firqatunnajia.com/uogaji-wa-kishariah-unamtosha-mtu-kutohitajia-kutawadha/ 

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (04) http://audio2.islamweb.net/lecturs/aalrrajhee/431/431.mp3
  • Imechapishwa: 09/07/2018