Swali: Ni ipi hukumu ya mwenye kusema wakati wa kuomba du´aa “Ee mpenzi” (يا حبيبي) akimkusudia Allaah?
Jibu: Hakuna neno. Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) ndiye mpenzi zaidi kwake. Lakini amuombe kwa majina Yake kama vile Allaah au Mwingi wa huruma (ar-Rahmaan) ndio bora zaidi. Kwa sababu Allaah (´Azza wa Jall) amesema:
وَلِلَّـهِ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ فَادْعُوهُ بِهَا
”Allaah ana majina mazuri mno. Hivyo basi muombeni kwayo.”[1]
Hakusema aombwe kwa jina la mpenzi. Muombe kwa majina na sifa Zake kama vile Allaah, Mwingi wa huruma na Mwenye utukufu mno na ukarimu (Dhul-Jalaal wal-Ikraam). Ijapokuwa yeye ndiye mpendwa zaidi. Lakini muombe kwa majina Yake aliyoyaweka wazi (Subhaanahu wa Ta´ala).
[1] 07:180
- Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Kashf-is-Shubuhaat, uk. 112
- Imechapishwa: 17/08/2019
Swali: Ni ipi hukumu ya mwenye kusema wakati wa kuomba du´aa “Ee mpenzi” (يا حبيبي) akimkusudia Allaah?
Jibu: Hakuna neno. Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) ndiye mpenzi zaidi kwake. Lakini amuombe kwa majina Yake kama vile Allaah au Mwingi wa huruma (ar-Rahmaan) ndio bora zaidi. Kwa sababu Allaah (´Azza wa Jall) amesema:
وَلِلَّـهِ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ فَادْعُوهُ بِهَا
”Allaah ana majina mazuri mno. Hivyo basi muombeni kwayo.”[1]
Hakusema aombwe kwa jina la mpenzi. Muombe kwa majina na sifa Zake kama vile Allaah, Mwingi wa huruma na Mwenye utukufu mno na ukarimu (Dhul-Jalaal wal-Ikraam). Ijapokuwa yeye ndiye mpendwa zaidi. Lakini muombe kwa majina Yake aliyoyaweka wazi (Subhaanahu wa Ta´ala).
[1] 07:180
Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Kashf-is-Shubuhaat, uk. 112
Imechapishwa: 17/08/2019
https://firqatunnajia.com/kumuomba-allaah-kwa-jina-la-mpenzi/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)