Swali: Nimemsikia Khatwiyb katika maimamu wa misikiti katika Khutbah ya pili katika Ramadhaan iliyobarikiwa akimjuzishia mfanya kazi aliyelazimika na wakati huohuo akawa hana kazi nyingine mbali na hii kwamba inatosha kutoa chakula kumlisha masikini kwa kila siku moja ya Ramadhaan. Je, haya yana dalili sahihi kutoka katika Qur-aan na Sunnah?
Jibu: Haijuzu kwa ambaye swawm inamuwajibikia kula mchana wa Ramadhaan kwa sababu tu eti ni mfanya kazi. Lakini akipata uzito mkubwa wenye kumpelekea kula mchana wa Ramadhaan basi atakula kiasi cha kuondosha uzito kisha baada ya hapo atajizuia mpaka wakati wa kuzama kwa jua. Jua likishazama atakula pamoja na wengine na atalipa siku hiyo aliyokula. Fatwa uliyotaja si sahihi.
´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
´Abdur-Razzaaq ´Afiyfiy
´Abdullaah al-Ghudayyaan
´Abdullaah bin Qu´uud
- Mhusika: al-Lajnah ad-Daa’imah
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa al-Ladjnah ad-Daa’imah (4157)
- Imechapishwa: 27/04/2020
Swali: Nimemsikia Khatwiyb katika maimamu wa misikiti katika Khutbah ya pili katika Ramadhaan iliyobarikiwa akimjuzishia mfanya kazi aliyelazimika na wakati huohuo akawa hana kazi nyingine mbali na hii kwamba inatosha kutoa chakula kumlisha masikini kwa kila siku moja ya Ramadhaan. Je, haya yana dalili sahihi kutoka katika Qur-aan na Sunnah?
Jibu: Haijuzu kwa ambaye swawm inamuwajibikia kula mchana wa Ramadhaan kwa sababu tu eti ni mfanya kazi. Lakini akipata uzito mkubwa wenye kumpelekea kula mchana wa Ramadhaan basi atakula kiasi cha kuondosha uzito kisha baada ya hapo atajizuia mpaka wakati wa kuzama kwa jua. Jua likishazama atakula pamoja na wengine na atalipa siku hiyo aliyokula. Fatwa uliyotaja si sahihi.
´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
´Abdur-Razzaaq ´Afiyfiy
´Abdullaah al-Ghudayyaan
´Abdullaah bin Qu´uud
Mhusika: al-Lajnah ad-Daa’imah
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fataawaa al-Ladjnah ad-Daa’imah (4157)
Imechapishwa: 27/04/2020
https://firqatunnajia.com/khatwiyb-akiwajuzishia-wafanya-kazi-kula-na-badala-yake-kutoa-chakula/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)