Waziri wa mambo ya Kiislamu Shaykh Swaalih Aal ash-Shaykh amewaonya wale wenye kujaribu kunasibisha ISIS na mfumo wa Salaf kwa kusema:

“Khawaarij walijitokeza katika Ummah wa watu bora, wakawaua watu bora kabisa na wakasoma kupitia mikono ya Maswahabah. Je, ni sahihi kusema kuwa Khawaarij ni mapando ya Maswahabah? Hapana, si sahihi. Kupatikana mambo mawili yaliyoambatana haina maana ya kwamba kimoja wapo ni natija ya chengine. Natija katika hali hii ni upotevu.”

  • Mhusika: ´Allaamah Swaalih bin ´Abdil-´Aziyz Aal ash-Shaykh
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://www.af.org.sa/ar/node/3717
  • Imechapishwa: 06/11/2016