Swali: Ni upi usahihi wa Hadiyth:
“Mwenye kunitembelea basi uombezi wangu umewajibika kwake”?
Jibu: Hadiyth hii ni dhaifu sana na imezuliwa. Si Swahiyh. Uombezi wa Mtuem (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) unapatikana kwa Tawhiyd na imani. Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) alisema hali ya kumuuliza:
“Ni nani mwenye furaha zaidi ya uombezi wako, ee Mtume wa Allaah?” Akasema: “Yule atakayesema ´hapana mungu wa haki isipokuwa Allaah` hali ya kuwa ni mtakasifu kutoka moyoni mwake.”
Jambo hili ni jepesi zaidi kuliko matembezi.
Kuhusu yule mwenye kutembelea kaburi lake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ilihali matendo yake ni maovu, ni mshirikina au ni mwenye kuendelea juu ya maasi au Bid´ah, hakika hayatomfaa kitu matembezi haya. Ama akimtembelea na huku ni mwenye kumpwekesha Allaah basi matembezi hayo yatamfaa.
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (12) https://audio.islamweb.net/audio/index.php?page=audioinfo&audioid=191546
- Imechapishwa: 29/09/2019
Swali: Ni upi usahihi wa Hadiyth:
“Mwenye kunitembelea basi uombezi wangu umewajibika kwake”?
Jibu: Hadiyth hii ni dhaifu sana na imezuliwa. Si Swahiyh. Uombezi wa Mtuem (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) unapatikana kwa Tawhiyd na imani. Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) alisema hali ya kumuuliza:
“Ni nani mwenye furaha zaidi ya uombezi wako, ee Mtume wa Allaah?” Akasema: “Yule atakayesema ´hapana mungu wa haki isipokuwa Allaah` hali ya kuwa ni mtakasifu kutoka moyoni mwake.”
Jambo hili ni jepesi zaidi kuliko matembezi.
Kuhusu yule mwenye kutembelea kaburi lake Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ilihali matendo yake ni maovu, ni mshirikina au ni mwenye kuendelea juu ya maasi au Bid´ah, hakika hayatomfaa kitu matembezi haya. Ama akimtembelea na huku ni mwenye kumpwekesha Allaah basi matembezi hayo yatamfaa.
Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (12) https://audio.islamweb.net/audio/index.php?page=audioinfo&audioid=191546
Imechapishwa: 29/09/2019
https://firqatunnajia.com/hapa-ndipo-matembezi-yatamfaa-mtu/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)