Endeleeni kufunga mpaka kuthibiti kinyume chake

Swali: Jana jioni tumesikia silaha za moto ambapo tukaingiwa na mashaka kama siku ya kufuata itakuwa ´iyd au Ramadhaan. Tulisubiri tusikie kitu kutoka kwa imamu katika Fajr, lakini hatukusikia chochote. Ni ipi hukumu ya kusita katika nia kati ya kufunga na kula?

Jibu: Ni lazima kwa mtu ahakikishe. Kimsingi ni kubaki kila kitu vile kilivyo. Kama kungelikuweko kitu basi kingedhihiri kwa njia ya kwamba ingelibainika kwa watu ili wasile daku na kufunga. Kwa hali yoyote siku hiyo bado inazingatiwa ni Ramadhaan. Mwezi ungelikuwa umemalizika basi mambo yangelikuwa wazi. Katika hali hiyo mtu analazimika kufunga pasi na shaka. Kwa sababu msingi ni kubaki kwa Ramadhaan. Siku ya kufuata ikibaini kiwa ni siku ya ´iyd, basi watafungua.

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (19/182-183)
  • Imechapishwa: 05/05/2021