Swali: Kuna mwanaume ana uwezo wa kimali na wa kimwili. Je, bora kwake kuoa mke mmoja peke yake au kuoa wake wengi?
Jibu: Kuoa wanawake wengi ndio bora zaidi kuliko kuoa mke mmoja tu. Hilo ni kwa sababu ya kule kukithirisha kizazi katika Ummah huu na kutokana vilevile na kuzihifadhi tupu za wanawake ambao hawana waume. Hilo ni kwa sharti zifuatazo:
1- Mtu awe na uwezo wa kimali.
2- Uwezo wa kimwili.
3- Uwezo wa kuitendaji. Namaanisha kuwafanyia uadilifu wanawake. Ama kuoa tu ilihali anachelea hatokuwa mwadilifu, hilo ni haramu juu yake. Allaah (Ta´ala) anasema:
فَإِنْ خِفْتُمْ أَلَّا تَعْدِلُوا فَوَاحِدَةً
“Mkichelea kuwa hamtoweza kufanya uadilifu, basi bakini na mmoja tu… “
Katika hali hii Allaah ameamrisha kubaki na mke mmoja tu.
أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُكُمْ
“… au ambao mikono yenu ya kulia imewamiliki.” (04:03)
Wanawake kama hawa – yaani masuriya – sio wajibu kufanya uadilifu kati yao. Anaweza kulala na amtakaye katika wanawake hawa – ikiwa yuko nao – na sio wajibu kufanya uadilifu. Kuhusu wake ni lazima kuwafanyia uadilifu.
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (11)
- Imechapishwa: 03/05/2020
Swali: Kuna mwanaume ana uwezo wa kimali na wa kimwili. Je, bora kwake kuoa mke mmoja peke yake au kuoa wake wengi?
Jibu: Kuoa wanawake wengi ndio bora zaidi kuliko kuoa mke mmoja tu. Hilo ni kwa sababu ya kule kukithirisha kizazi katika Ummah huu na kutokana vilevile na kuzihifadhi tupu za wanawake ambao hawana waume. Hilo ni kwa sharti zifuatazo:
1- Mtu awe na uwezo wa kimali.
2- Uwezo wa kimwili.
3- Uwezo wa kuitendaji. Namaanisha kuwafanyia uadilifu wanawake. Ama kuoa tu ilihali anachelea hatokuwa mwadilifu, hilo ni haramu juu yake. Allaah (Ta´ala) anasema:
فَإِنْ خِفْتُمْ أَلَّا تَعْدِلُوا فَوَاحِدَةً
“Mkichelea kuwa hamtoweza kufanya uadilifu, basi bakini na mmoja tu… ”
Katika hali hii Allaah ameamrisha kubaki na mke mmoja tu.
أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُكُمْ
“… au ambao mikono yenu ya kulia imewamiliki.” (04:03)
Wanawake kama hawa – yaani masuriya – sio wajibu kufanya uadilifu kati yao. Anaweza kulala na amtakaye katika wanawake hawa – ikiwa yuko nao – na sio wajibu kufanya uadilifu. Kuhusu wake ni lazima kuwafanyia uadilifu.
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Liqaa’ ash-Shahriy (11)
Imechapishwa: 03/05/2020
https://firqatunnajia.com/bora-kuoa-mke-mmoja-au-wengi-%e2%80%82%e2%80%82%e2%80%82%e2%80%82/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)