ar-Raajihiy kuhusu pete ya uchumba au ya ndoa

Swali: Ni ipi hukumu mwanaume kumvisha mchumba wake pete ya ndoa au ad-Dublah? Nimesikia kwamba jambo hilo ni kujifananisa na manaswara[1].

Jibu: Ikiwa ni kujifananisha basi ni haramu na wala haifai. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Mwenye kujifananisha watu basi yeye ni katika wao.”

Kadhalika ikiwa ni katikati ya wanawake basi kitendo hichi ni uchache wa haya kwa kule kukaa kwake mbele ya wanawake. Ama akiionyesha mbele ya wanaume ndio kitendo hichi ndio khatari zaidi. Haifai ikiwa ni kujifananisha. Pia ni haramu kutokana na ule uchache wa haya ulio ndani yake.

[1] Tazama https://firqatunnajia.com/46-maovu-ya-sita-pete-ya-uchumba/

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (09) http://audio.islamweb.net/audio/index.php?page=FullContent&audioid=191370#219699
  • Imechapishwa: 30/03/2019