´Amr Khaalid sio mwanachuoni. Hana jipya la kuja nalo. Ni mtu taabani. Hali yake inasikitisha. Anapokelewa na nchi kwenye viwanja vya ndege. Huenda nchi hizi ni shinikizo la Marekani wampokee. Alikuja Yemen na akapokelewa rasmi. Akaanza kutoa mihadhara. Wanamume kwa wanawake walikuwa wamekusanyika sehemu moja. Wanaweka kiwango kikubwa cha pesa. Tiketi moja ilikuwa ngapi? Mnakumbuka tiketi moja ilikuwa inauzwa ngapi? Ni pesa nyingi. Amevaa tai. Amenyoa ndevu. Amevaa koti. Anawachekesha watu. Anauliza ni nani mwenye kusema kuwa shaytwaan ni kafiri. Anasema kuwa Ibliys sio kafiri. Anawachezea shere watu kiasi hichi. Ameyasema haya kwa lahja yake ya kimisri na kwamba sio kafiri. Ilihali Allaah anasema:

إِلَّا إِبْلِيسَ أَبَىٰ وَاسْتَكْبَرَ وَكَانَ مِنَ الْكَافِرِينَ

”… isipokuwa Ibliys alikataa na akatakabari na akawa miongoni mwa makafiri.” (02:34)

Anamtetea shaytwaan, Ibliys, na kusema kuwa sio kafiri. Hii ina maana gani? Anataka kuwafanya waislamu kuwa na mashaka juu ya Qur-aan? Je, tuyakubali maneno yake ya batili na kuyarudishe maneno ya Allaah?

Anasema kitu kuhusu kwamba Nabii Daawuud aliichukua ardhi iliyoko chini ya msikiti Yerusalemu, iliyokuwa ya mwanamke wa kiyahudi, kwa nguvu. Hii ina maana kuwa yuko pamoja na mayahudi na manaswara.

  • Mhusika: ´Allaamah Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab al-Wasswaabiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://www.darulhadith.com/v2/var-star-%C2%B4amr-khalid-egentligen/
  • Imechapishwa: 09/04/2017