Swali: Je, majina ya Allaah yameumbwa?

Jibu: Majina na sifa za Allaah hazikuumbwa. Allaah kwa dhati, majina na sifa Zake ndiye muumba na vyenginevyo vimeumbwa.

Mwenye kusema kuwa maneno ya Allaah na sifa Zake zimeumbwa ni ukafiri. Hivo ndivo walivosema maimamu kama Imaam Ahmad na wengineo. Amesema:

“Mwenye kusema kuwa Qur-aan imeumbwa ni ukafiri.”

Inapokuja kwa mtu mmojammoja basi hakufurishwi mpaka asimamishiwe hoja kwanza. Lakini kwa njia ya ujumla ni kwamba yule mwenye kusema kuwa maneno na sifa za Allaah zimeumbwa ni ukafiri. Tunamuomba Allaah afya.

  • Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajihiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Fataawaa Mutanawwi´ah (14) https://audio.islamweb.net/audio/index.php?page=audioinfo&audioid=191634
  • Imechapishwa: 05/04/2020