Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
Katika Hadiyth:
“Kichwa cha mambo ni Uislamu, nguzo yake ni swalah na jihaad katika njia ya Allaah ndio nundu yake ya juu.”[1]
MAELEZO
Mtunzi wa kitabu (Rahimahu Allaah) anachokusudia kwa Hadiyth hii ni kuonesha kuwa kila kitu kina kichwa cha mambo. Kichwa cha mambo alichokuja nacho Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni Uislamu.
… nguzo yake ni swalah – Kwa sababu Uislamu hausimami isipokuwa kwayo. Kwa ajili hii maoni yenye nguvu ni kwamba yule mwenye kuacha swalah ni kafiri na hana Uislamu wowote.
Jihaad katika njia ya Allaah ndio nundu yake ya juu – Bi maana mambo yake ya juu na kamilifu zaidi ni kupambana jihaad katika njia ya Allaah. Hili ni kutokana na kwamba yule mwenye kuitengeneza nafsi yake ajaribu pia kuwatengeneza wengine kupitia jihaad katika njia ya Allaah. Hili hufanywa ili Uislamu uweze kusimamishwa na ili neno la Allaah liweze kuwa juu. Yule mwenye kupambana ili neno la Allaah liweze kuwa juu, basi huyo ndiye mwenye kupambana katika njia ya Allaah. Kwa hivyo ndio hufikiwa nundu hii ya juu kwa sababu ni kupitia yenyewe ndio Uislamu unakuwa juu ya dini nyinginezo.
[1] Ahmad (5/231-237), at-Tirmidhiy (5/13) na Ibn Maajah (2/1394).
- Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Thalaathat-il-Usuwl, uk. 160
- Imechapishwa: 05/06/2020
Shaykh-ul-Islaam Muhammad bin ´Abdil-Wahhaab (Rahimahu Allaah) amesema:
Katika Hadiyth:
“Kichwa cha mambo ni Uislamu, nguzo yake ni swalah na jihaad katika njia ya Allaah ndio nundu yake ya juu.”[1]
MAELEZO
Mtunzi wa kitabu (Rahimahu Allaah) anachokusudia kwa Hadiyth hii ni kuonesha kuwa kila kitu kina kichwa cha mambo. Kichwa cha mambo alichokuja nacho Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni Uislamu.
… nguzo yake ni swalah – Kwa sababu Uislamu hausimami isipokuwa kwayo. Kwa ajili hii maoni yenye nguvu ni kwamba yule mwenye kuacha swalah ni kafiri na hana Uislamu wowote.
Jihaad katika njia ya Allaah ndio nundu yake ya juu – Bi maana mambo yake ya juu na kamilifu zaidi ni kupambana jihaad katika njia ya Allaah. Hili ni kutokana na kwamba yule mwenye kuitengeneza nafsi yake ajaribu pia kuwatengeneza wengine kupitia jihaad katika njia ya Allaah. Hili hufanywa ili Uislamu uweze kusimamishwa na ili neno la Allaah liweze kuwa juu. Yule mwenye kupambana ili neno la Allaah liweze kuwa juu, basi huyo ndiye mwenye kupambana katika njia ya Allaah. Kwa hivyo ndio hufikiwa nundu hii ya juu kwa sababu ni kupitia yenyewe ndio Uislamu unakuwa juu ya dini nyinginezo.
[1] Ahmad (5/231-237), at-Tirmidhiy (5/13) na Ibn Maajah (2/1394).
Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Sharh Thalaathat-il-Usuwl, uk. 160
Imechapishwa: 05/06/2020
https://firqatunnajia.com/89-kichwa-cha-mambo-ni-uislamu/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)