70. al-´Ayyaashiy upotoshaji wake wa kumi na moja wa Aal ´Imraan

al-´Ayyaashiy amesema:

“Hammaad bin ´Iysaa amepokea kutoka kwa baadhi ya marafiki zake, kutoka kwa Abu ´Abdillaah aliyesema: “Pindi ´Aliy (Radhiya Allaahu ´anh) aliposoma:

كُنتُمْ خَيْرَ أُمَّةٍ أُخْرِجَتْ لِلنَّاسِ

“Mmekuwa ni Ummah bora kabisa uliotolewa [katika na] kwa watu.”[1]

kisha akasema: “Ni familia ya Muhammad (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).”

Abu Baaswiyr amepokea ya kwamba amesema: “Aayah hii imeteremka juu ya Muhammad kuhusiana na yeye na wausiwa na si mwingine. Akasema:

كُنتُمْ خَيْرَ أئمّةٍ أُخْرِجَتْ لِلنَّاسِ

“Mmekuwa ni maimamu bora kabisa uliotolewa [katika na] kwa watu.”

Ninaapa kwa Allaah ya kwamba iliteremshwa namna hii na Jibriyl. Hakuna waliolengwa isipokuwa Muhammad na wausiwa.”[2]

Namna hii unaona namna ambavyo Raafidhwah wanaita katika maovu makubwa. Wanakipotosha kitabu cha Allaah kwa ujasiri wote. Si mayahudi wala watu wengine hawawezi kufanya kitu kama hicho.

Allaah amemtakasa Muhammad, Jibriyl, waislamu na familia ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kutokamana na uongo huu na upotoshaji wa khatari. Hakuna mwingine zaidi ya shaytwaan aliyewatemremshia wapenzi wake, wanusuraji wake na majeshi yake katika Raafidhwah Baatwiniyyah.

[1] 03:110

[2] Tafsiyr al-´Ayyaashiy (1/195).

  • Mhusika: ´Allaamah Rabiy´ bin Haadiy al-Madkhaliy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Intiswaar li Kitaab-il-´Aziyz al-Jabbaar, uk. 106-107
  • Imechapishwa: 03/04/2017