13 – Mwanamke atapunguza nywele za kichwani mwake kwa ajili ya hajj na ´umrah kwa kiasi cha ncha ya kidole. Haijuzu kwake kunyoa. Ncha ya kidole ni kichwa cha kidole katika tindi yake ya juu. Mtunzi wa “al-Mughniy” amesema:
“Kilichosuniwa kwa mwanamke ni kupunguza nywele na si kunyoa na hakuna tofauti juu ya hilo. Ibn-ul-Mundhir amesema: “Wanachuoni wameafikiana juu ya hilo kwa sababu kunyoa juu yao ni kukatwakatwa. Ibn ´Abbaas amepokea kwa kusema: “Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Wanawake hawana kunyoa. Kilichoko kwa wanawake ni kupunguza.”
Ameipokea Abu Daawuud.
´Aliy amesimulia:
“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amekataza mwanamke kunyoa kichwa chake.”
Ameipokea Abu Daawuud.
Ahmad alikuwa akisema:
“Apunguze kwa kila fundo kiasi cha tindi ya juu ya kidole.”
Hayo pia ndio maoni ya Ibn ´Umar, ash-Shaafi´iy, Ishaaq na Abu Thawr.
Abu Daawuud amesema:
“Nimemsikia Ahmad akiulizwa kama mwanamke apunguze nywele zake zote?” Akajibu: “Ndio. Atazikusanya nywele zake mpaka mbele ya kichwa chake kisha atakata katika ncha ya nywele zake kiasi cha tindi ya juu ya kidole.”[1]
Imaam an-Nawawiy amesema katika “al-Majmuu´”:
“Wanachuoni wameafikiana kwamba mwanamke hakuamrishwa kunyoa. Bali kazi yake ni yeye kupunguza nywele za kichwani mwake. Kwa sababu ni Bid´ah juu yao na kukatwakatwa.”[2]
[1] (05/310).
[2] (08/150-154).
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Tanbiyhaat, uk. 94-95
- Imechapishwa: 14/11/2019
13 – Mwanamke atapunguza nywele za kichwani mwake kwa ajili ya hajj na ´umrah kwa kiasi cha ncha ya kidole. Haijuzu kwake kunyoa. Ncha ya kidole ni kichwa cha kidole katika tindi yake ya juu. Mtunzi wa “al-Mughniy” amesema:
“Kilichosuniwa kwa mwanamke ni kupunguza nywele na si kunyoa na hakuna tofauti juu ya hilo. Ibn-ul-Mundhir amesema: “Wanachuoni wameafikiana juu ya hilo kwa sababu kunyoa juu yao ni kukatwakatwa. Ibn ´Abbaas amepokea kwa kusema: “Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Wanawake hawana kunyoa. Kilichoko kwa wanawake ni kupunguza.”
Ameipokea Abu Daawuud.
´Aliy amesimulia:
“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amekataza mwanamke kunyoa kichwa chake.”
Ameipokea Abu Daawuud.
Ahmad alikuwa akisema:
“Apunguze kwa kila fundo kiasi cha tindi ya juu ya kidole.”
Hayo pia ndio maoni ya Ibn ´Umar, ash-Shaafi´iy, Ishaaq na Abu Thawr.
Abu Daawuud amesema:
“Nimemsikia Ahmad akiulizwa kama mwanamke apunguze nywele zake zote?” Akajibu: “Ndio. Atazikusanya nywele zake mpaka mbele ya kichwa chake kisha atakata katika ncha ya nywele zake kiasi cha tindi ya juu ya kidole.”[1]
Imaam an-Nawawiy amesema katika “al-Majmuu´”:
“Wanachuoni wameafikiana kwamba mwanamke hakuamrishwa kunyoa. Bali kazi yake ni yeye kupunguza nywele za kichwani mwake. Kwa sababu ni Bid´ah juu yao na kukatwakatwa.”[2]
[1] (05/310).
[2] (08/150-154).
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Tanbiyhaat, uk. 94-95
Imechapishwa: 14/11/2019
https://firqatunnajia.com/47-hukumu-kuhusu-mwanamke-kupunguza-nywele-zake/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)