4. Sababu ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kutoendelea kuswali mkusanyiko

[5] Sababu iliyomfanya (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kutoendelea kuswali na wao mkusanyiko mwezi uliobaki, ilikuwa ni kuchelea swalah za nyusiku zisije kufaradhishwa kwao katika Ramadhaan. Hiki ni kitu wasingekiweza, kama ilivyotajwa katika Hadiyth ya ´Aaishah katika “as-Swahiyh” ya al-Bukhaariy na Muslim na vyenginevyo[1]. Wasiwasi huu uliondoka kwa kufa kwake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) baada ya Allaah kukamilisha Shari´ah na kwa ajili hiyo mtu alikuwa anaweza kurudi kuswali nyusiku za Ramadhaan kwa mkusanyiko. Hukumu ya asili ikawa imebaki, ambayo ni kuswali kwa mkusanyiko, na kwa ajili hiyo ndio maana ´Umar (Radhiya Allaahu ´anh) akaihuisha, kama ilivyotajwa katika “as-Swahiyh” ya al-Bukhaariy na vyenginevyo[2].

[1] Tazama “at-Taraawiyh”, uk. 12-14.

[2] Tazama takhriyj ya Hadiyth hii na maneno ya Ibn ´Abdil-Barr na wengineo juu yake katika marejeo yaliyotangulia, uk. 49-52.

  • Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Qiyaam Ramadhwaan, uk. 21
  • Imechapishwa: 07/05/2019