4- Kufunga jumatatu na alkhamisi kila wiki. ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) amesimulia:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akitilia umuhimu funga ya jumatatu na alkhamisi.”[1]
Vilevile amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Matendo huonyeshwa jumatatu na alkhamisi. Hivyo napenda yaonyeshwe matendo yangu nami nimefunga.”[2]
5- Kufunga siku tatu kila mwezi. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kumwambia ´Abdullaah bin ´Amr:
“Funga katika mwezi siku tatu. Kwani hakika jema moja linalipwa mara kumi mfano wake na hivyo ni kama kufunga mwaka mzima.”
Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Aliniusia kipenzi changu mambo matatu; kufunga siku tatu kila mwezi, Rak´ah mbili za Dhuhaa´ na kuswali Witr kabla ya kulala.”
Masiku hayo yamependekezwa yawe yale meupe; tarehe 13, 14 na 15. Abu Dharr (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Yule katika nyinyi mwenye kufunga katika mwezi basi afunge siku tatu nyeupe.”
6- Kufunga siku moja na kuacha ya kufuata. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Swawm bora ni ya Daawuud (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Alikuwa akifunga siku moja na akila ya kufuata.”
Hii ndio funga iliyopendekezwa ambayo ni bora zaidi.
[1] Ahmad (05/201) na at-Tirmidhiy (745) ambaye amesema:
“Nzuri na Swahiyh”.
Ameisahihisha al-Albaaniy katika “Ta´liyq ´alaa Ibn Khuzaymah” (2116).
[2] at-Tirmidhiy (751), an-Nasaa´iy (01/322), Abu Daawud (2432). Ni Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Swahiyh-ut-Tirmidhiy” (596).
- Mhusika: Nukhbatin minal-´Ulamaa´
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fiqh-ul-Muyassar, uk. 162-163
- Imechapishwa: 01/05/2020
4- Kufunga jumatatu na alkhamisi kila wiki. ´Aaishah (Radhiya Allaahu ´anhaa) amesimulia:
“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akitilia umuhimu funga ya jumatatu na alkhamisi.”[1]
Vilevile amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Matendo huonyeshwa jumatatu na alkhamisi. Hivyo napenda yaonyeshwe matendo yangu nami nimefunga.”[2]
5- Kufunga siku tatu kila mwezi. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kumwambia ´Abdullaah bin ´Amr:
“Funga katika mwezi siku tatu. Kwani hakika jema moja linalipwa mara kumi mfano wake na hivyo ni kama kufunga mwaka mzima.”
Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:
“Aliniusia kipenzi changu mambo matatu; kufunga siku tatu kila mwezi, Rak´ah mbili za Dhuhaa´ na kuswali Witr kabla ya kulala.”
Masiku hayo yamependekezwa yawe yale meupe; tarehe 13, 14 na 15. Abu Dharr (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Yule katika nyinyi mwenye kufunga katika mwezi basi afunge siku tatu nyeupe.”
6- Kufunga siku moja na kuacha ya kufuata. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Swawm bora ni ya Daawuud (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Alikuwa akifunga siku moja na akila ya kufuata.”
Hii ndio funga iliyopendekezwa ambayo ni bora zaidi.
[1] Ahmad (05/201) na at-Tirmidhiy (745) ambaye amesema:
“Nzuri na Swahiyh”.
Ameisahihisha al-Albaaniy katika “Ta´liyq ´alaa Ibn Khuzaymah” (2116).
[2] at-Tirmidhiy (751), an-Nasaa´iy (01/322), Abu Daawud (2432). Ni Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Swahiyh-ut-Tirmidhiy” (596).
Mhusika: Nukhbatin minal-´Ulamaa´
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fiqh-ul-Muyassar, uk. 162-163
Imechapishwa: 01/05/2020
https://firqatunnajia.com/23-swawm-zilizopendekezwa-ii/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)