4-

اللَّهُمَّ بِعِلْمِكَ الْغَيْبَ وَقُدْرَتِكَ على الْخَلْقِ أَحْيِني ما عَلِمْتَ الْحَيَاةَ خَيْراً لِي وَتَوفَّني إِذَا عَلِمْتَ الْوَفَاةَ خَيْراً لِي اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ خَشْيَتَكَ في الْغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ وَأَسْأَلُكَ كَلِمَةَ الْحَقِّ في الرِّضَا وَ الْغَضبِ وَأَسْأَلُكَ الْقَصدَ في الْفَقْرِ والْغِنى وَأَسْأَلُكَ نَعِيماً لاَ يَنْفَدُ وَأَسْأَلُكَ قُرَّةَ عَيْنٍ لاَ تَنْقَطع وَأَسْأَلُكَ الرِّضَا بَعْدَ الْقَضَاءِ وَأَسْأَلُكَ بَرْدَ الْعَيْشِ بعد الْمَوتِ وَأَسْأَلكَ لَذَّةَ النَّظرِ إِلى وَجْهِكَ والشَّوْقَ إِلى لِقَائِكَ في غيرِ ضَرَّاءَ مُضِرَّةٍ وَلاَ فِتْنَةٍ مُضِلَّةٍ اللَّهُمَّ زَيِّنَّا بِزِينةِ الإِيْمانِ وَاجْعَلْنَا هُدَاةً مُهْتَدِينَ

“Ee Allaah! Nakuomba kwa ujuzi Wako wa yaliyofichikana na uwezo Wako juu ya kuumba. Nifanye kuwa hai muda wa kuwa Unajua kwamba uhai ni bora kwangu. Nifishe muda wa kuwa unajua kuwa kufa ni bora kwangu. Ee Allaah! Hakika mimi nakuomba kukuogopa kwa siri na kwa dhahiri. Nakuomba kutamka neno la haki wakati furaha na wakati kukasirika. Nakuomba matumizi ya wastani wakati wa umasikini na wakati wa utajiri. Nakuomba neema isiyokatika. Nakuomba kituliza jicho kisichokatika. Nakuomba kuridhia baada ya kuwa umeshanipangia. Nakuomba maisha mazuri baada ya kufa. Nakuomba ladha ya kukutizama uso Wako na shauku ya kukutana Nawe pasi na madhara yanayodhuru wala fitina yenye kupoteza. Ee Allaah! Tupambe kwa pambo la imani na tufanye tuwe waongozi wenye kuongoka.”[1]

[1] an-Nasaa’iy na al-Haakim ameisahihisha na adh-Dhahabiy akaafikiana naye.

  • Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Swifatu Swalaat-in-Nabiy, uk. 160
  • Imechapishwa: 10/01/2019