Mwishoni namwambia Shaykh Bakr na wengine kwamba nimetumia juhudi kubwa kupata tawbah ya wazi, ya kweli juu ya fikira na I´tiqaad za Sayyid Qutwub na sikupata kitu. Nikilipata hilo, basi nitajirejea kumkosoa. Katika hali hii ni wajibu kumlaumu na kumuadhibu yule mwenye kuficha tawbah yake ya kweli na badala yake anaeneza I´tiqaad zake mbovu na zilizofutwa.

Lau tawbah na urejeaji wa wazi na wa kweli utakosekana, basi ni juu ya Shaykh Bakr na wengine wote walio na msimamo wa kupindukia kwa Sayyid Qutwub wastahi kwa Allaah na kwa waislamu wenye busara wanaoziheshimu akili zao. Wasiuudhi Uislamu na Ummah. Wasicheze na akili za vijana na kuwafanya wakashikamana na batili na kupiga vita haki na watu wa haki. Watubie kwa Allaah kwa kuwalea vijana kuwa na ukaidi na inadi.

Kadhadlika wanatakiwa waheshimu Uislamu wao, dhamira zao na akili zao. Wanatakiwa pia kuheshimu mfumo wa Uislamu ambao unalea wanaume, kuipenda na kuiheshimu haki na kuichukia na kuitweza batili na watu wake na kutahadhari na shari, fitina na njama zao.