Haya yanatakiwa kutambulika. Mapote yote, ya zamani na ya sasa, ni wenye kutilia mkazo Tawhiyd-ur-Rubuubiyyah. Kwa mujibu wao wanaona kuwa mja anakuwa muislamu kwa sababu tu anakubali kuwa Allaah ndiye Muumbaji na Mruzukaji. Hivo ndivo wameandika ´Aqiydah zao kwenye vitabu. Vitabu vya wanafalsafa vinazungumzia tu Tawhiyd-ur-Rubuubiyyah na dalili zake. Haya hayatoshi. ´Ibaadah ni jambo la lazima. Amesema (Ta´ala):
وَلَقَدْ بَعَثْنَا فِي كُلِّ أُمَّةٍ رَّسُولًا أَنِ اعْبُدُوا اللَّـهَ وَاجْتَنِبُوا الطَّاغُوتَ
”Hakika Tulituma katika kila ummah Mtume kwamba: “Mwabuduni Allaah na jiepusheni na Twaaghuut [waungu batili].”[1]
Wakiwaamrisha watu kumwabudu Allaah. Hii ndio Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah:
وَمَا أَرْسَلْنَا مِن قَبْلِكَ مِن رَّسُولٍ إِلَّا نُوحِي إِلَيْهِ أَنَّهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا أَنَا فَاعْبُدُونِ
“Hatukutuma kabla yako Mtume yeyote isipokuwa Tulimfunulia Wahy ya kwamba: “Hakika hapana mwabudiwa wa haki isipokuwa Mimi; hivyo basi niabuduni.”[2]
وَاعْبُدُوا اللَّـهَ وَلَا تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا
“Mwabuduni Allaah na wala msimshirikishe Yeye na chochote.”[3]
Aayah zote zinaamrisha na kuita katika Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah. Mitume wote walilingania katika Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah, wakawaamrisha nyumati zao na wakawakataza shirki. Hili ndilo kusudio na lengo la Tawhiyd.
Ama kuhusu Tawhiyd-ul-Asmaa´ was-Swifaat, inapingwa na wazushi kama Jahmiyyah, Mu´tazilah na Ashaa´irah pamoja na kutofautiana kwao katika jambo hilo.
[1] 16:36
[2] 21:25
[3] 04:36
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: at-Ta´liyqaat al-Mukhtaswarah ´alaal-´Aqiydah at-Twahaawiyyah, uk. 31-32
- Imechapishwa: 04/06/2019
Haya yanatakiwa kutambulika. Mapote yote, ya zamani na ya sasa, ni wenye kutilia mkazo Tawhiyd-ur-Rubuubiyyah. Kwa mujibu wao wanaona kuwa mja anakuwa muislamu kwa sababu tu anakubali kuwa Allaah ndiye Muumbaji na Mruzukaji. Hivo ndivo wameandika ´Aqiydah zao kwenye vitabu. Vitabu vya wanafalsafa vinazungumzia tu Tawhiyd-ur-Rubuubiyyah na dalili zake. Haya hayatoshi. ´Ibaadah ni jambo la lazima. Amesema (Ta´ala):
وَلَقَدْ بَعَثْنَا فِي كُلِّ أُمَّةٍ رَّسُولًا أَنِ اعْبُدُوا اللَّـهَ وَاجْتَنِبُوا الطَّاغُوتَ
”Hakika Tulituma katika kila ummah Mtume kwamba: “Mwabuduni Allaah na jiepusheni na Twaaghuut [waungu batili].”[1]
Wakiwaamrisha watu kumwabudu Allaah. Hii ndio Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah:
وَمَا أَرْسَلْنَا مِن قَبْلِكَ مِن رَّسُولٍ إِلَّا نُوحِي إِلَيْهِ أَنَّهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا أَنَا فَاعْبُدُونِ
“Hatukutuma kabla yako Mtume yeyote isipokuwa Tulimfunulia Wahy ya kwamba: “Hakika hapana mwabudiwa wa haki isipokuwa Mimi; hivyo basi niabuduni.”[2]
وَاعْبُدُوا اللَّـهَ وَلَا تُشْرِكُوا بِهِ شَيْئًا
“Mwabuduni Allaah na wala msimshirikishe Yeye na chochote.”[3]
Aayah zote zinaamrisha na kuita katika Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah. Mitume wote walilingania katika Tawhiyd-ul-Uluuhiyyah, wakawaamrisha nyumati zao na wakawakataza shirki. Hili ndilo kusudio na lengo la Tawhiyd.
Ama kuhusu Tawhiyd-ul-Asmaa´ was-Swifaat, inapingwa na wazushi kama Jahmiyyah, Mu´tazilah na Ashaa´irah pamoja na kutofautiana kwao katika jambo hilo.
[1] 16:36
[2] 21:25
[3] 04:36
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: at-Ta´liyqaat al-Mukhtaswarah ´alaal-´Aqiydah at-Twahaawiyyah, uk. 31-32
Imechapishwa: 04/06/2019
https://firqatunnajia.com/07-tawhiyd-kwa-mujibu-wa-ahl-ul-bidah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)