Wanandoa wote wawili wakiwa ni wasafiri wakati wamefunga. Kisha baadaye wakataka kufanya jimaa. Itafaa? Ndio, itafaa wakaanya jimaa kwa sababu msafiri halazimiki kufunga. Kwa hiyo ikiwa mume na mke wamesfiri kwenda Makkah kufanya ´Umrah na baadaye wakataka kufanya jimaa, wana ruhusa ya kufanya hivo. Aidha hawahitajii kutoa kafara na wala hawapati dhambi. Lakini watalipa siku nyingine badala ya siku hiyo baada ya Ramadhaan.

Huenda wanandoa wawili wamefunga na wako nyumbani na mume akataka kufanya jimaa lakini hata hivyo mke akakataa. Je, inafaa mke akamkatalia? Si kwamba inafaa tu bali ni lazima kwake kumkatalia. Lakini akimlazimisha kufanya jimaa na mke akashindwa kumzuia na hatimaye akamjamii, mume anapata dhambi kwa njia mbili:

1- Ameiharibu swawm yake.

2- Amemlazimisha jimaa mke wake.

Kuhusu mke yeye hapati dhambi. Hahitajii kulipa siku hiyo wala kutoa kafara kwa sababu ni mwenye kupewa udhuru.

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: ash-Sharh al-Mukhtaswar ´alaa Buluugh-il-Maraam (2/422)
  • Imechapishwa: 26/04/2020