Swali: Mwaka uliyopita nilihiji mimi na mume wangu. Siku ya ´Arafah mume wangu alipoteana nami na hatukuonana isipokuwa baada ya kumalizika hajj nchini kwetu. Je, hajj yangu ni sahihi au ni pungufu?
Jibu: Hajj ni sahihi. Haina upungufu wowote. Allaah (Tabaarak wa Ta´ala) amesema:
فَاتَّقُوا اللَّـهَ مَا اسْتَطَعْتُمْ
”Mcheni Allaah muwezavyo.”[1]
لَا يُكَلِّفُ اللَّـهُ نَفْسًا إِلَّا وُسْعَهَا
”Allaah hakalifishi nafsi yoyote isipokuwa kwa kadiri ya uwezo wake.”[2]
Afanye nini akimkosa mume wake? Aendelee kufanya hajj yake na arudi pamoja na marafiki zake.
[1] 64:16
[2] 02:286
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Liqaa´ ash-Shahriy (63) http://binothaimeen.net/content/1427
- Imechapishwa: 07/07/2020
Swali: Mwaka uliyopita nilihiji mimi na mume wangu. Siku ya ´Arafah mume wangu alipoteana nami na hatukuonana isipokuwa baada ya kumalizika hajj nchini kwetu. Je, hajj yangu ni sahihi au ni pungufu?
Jibu: Hajj ni sahihi. Haina upungufu wowote. Allaah (Tabaarak wa Ta´ala) amesema:
فَاتَّقُوا اللَّـهَ مَا اسْتَطَعْتُمْ
”Mcheni Allaah muwezavyo.”[1]
لَا يُكَلِّفُ اللَّـهُ نَفْسًا إِلَّا وُسْعَهَا
”Allaah hakalifishi nafsi yoyote isipokuwa kwa kadiri ya uwezo wake.”[2]
Afanye nini akimkosa mume wake? Aendelee kufanya hajj yake na arudi pamoja na marafiki zake.
[1] 64:16
[2] 02:286
Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Liqaa´ ash-Shahriy (63) http://binothaimeen.net/content/1427
Imechapishwa: 07/07/2020
https://firqatunnajia.com/vipi-hajj-ya-mwanamke-ambaye-amepoteana-na-mumewe/