Swali: Mwaka uliyopita nilihiji mimi na mume wangu. Siku ya ´Arafah mume wangu alipoteana nami na hatukuonana isipokuwa baada ya kumalizika hajj nchini kwetu. Je, hajj yangu ni sahihi au ni pungufu?
Jibu: Hajj ni sahihi. Haina upungufu wowote. Allaah (Tabaarak wa Ta´ala) amesema:
فَاتَّقُوا اللَّـهَ مَا اسْتَطَعْتُمْ
”Mcheni Allaah muwezavyo.”[1]
لَا يُكَلِّفُ اللَّـهُ نَفْسًا إِلَّا وُسْعَهَا
”Allaah hakalifishi nafsi yoyote isipokuwa kwa kadiri ya uwezo wake.”[2]
Afanye nini akimkosa mume wake? Aendelee kufanya hajj yake na arudi pamoja na marafiki zake.
[1] 64:16
[2] 02:286
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Liqaa´ ash-Shahriy (63) http://binothaimeen.net/content/1427
- Imechapishwa: 07/07/2020
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket