Uso ulioharibiwa kwenye vitabu na kuweka msitari shingoni

Swali: Je, ni lazima kuharibu picha zilizo kwenye vitabu? Je, ule uharamu unaondoka kwa kuweka msitari shingoni au kwenye mwili?

Jibu: Sioni kuwa kuna ulazima wa kufanya hivo, kwa sababu kuna uzito mkubwa wa kufanya hivo. Aidha ni kwamba vitabu hivi havikukusudia picha hizo, vimekusudia ile elimu iliyomo ndani yake. Kuweka msitari shingoni au kwenye mwili hakubadilishi uhalisia wa picha.

  • Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (12/343)
  • Imechapishwa: 12/04/2026