´Aliy bin Abiy Twaalib (Radhiya Allaahu ´anhu) ameeleza:

”Kuna mtumwa mmoja alikuja na kujaribu kujinunua huru kwake na kusema: “Mimi siwezi nashindwa kujinunua huru. Nisaidie.” Akasema: “Nisikufunze maneno aliyonifunza Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)? Lau utakuwa na deni mfano wa jibali Allaah Atakulipia nalo. Sema:

اللهُمَّ اكْفِنِي بِحَلاَلِكَ عنْ حَرامِكَ وأَغْنِنِي بِفَضْلِكَ عَمَّنْ سوَاكَ

“Ee Allaah! Nitosheleze mimi kwa halali yako kutokana na haramu yako. Nitajirishe kwa fadhilah zako nisiwahitaji wengine usio Wewe.”[1]

Ameipokea at-Tirmidhiy, ambaye amesema:

”Hadiyth ni nzuri.”

[1] at-Tirmidhiy (3563), Ahmad (1/424) na al-Haakim (1/538), ambaye ameisahihisha na imenyamaziwa na adh-Dhahabiy. Nzuri kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Swahiyh-ul-Kalim at-Twayyib” (116).

  • Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Abiy Bakr bin Qayyim-il-Jawziyyah (afk. 751)
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Waabil as-Swayyib wa Raafi´-ul-Kalim at-Twayyib, uk. 309
  • Imechapishwa: 22/09/2025