Swali: Nilioa mwanamke nikabaki nae kwa muda, kisha nikamtaliki na akaolewa na mwanaume mwingine baada yangu. Je, inajuzu kwake kumbusu na kumsalimia baba yangu baadaya kumtaliki?
Ibn Baaz: Hakuna ubaya. Kwa kuwa Allaah Kasema:
وَحَلَائِلُ أَبْنَائِكُمُ
“Na (mmeharamishwa) wake wa watoto wenu.” (04:23)
Ni katika wake wa watoto (walioharamishwa kwa baba). Hata kama amemtaliki. Ni Mahram wa baba yako.
Muulizaji: Yaani umahram wao ni wenye kubaki hata kama amemtaliki?
Ibn Baaz: Ni kama mke wa baba yake, lau baba yake atamtaliki, bado (mama huyo) ataendelea kuwa Mahram wake (mtoto). Allaah Kasema:
وَلَا تَنكِحُوا مَا نَكَحَ آبَاؤُكُم مِّنَ النِّسَاءِ
“Na wala msiwaoe (wake) waliowaoa baba zenu.” (04:22)
Baba akimtaliki (mke wake) au mtoto (mke wake), anakuwa ni Haraam (huyu kwa yule, na yule kwa huyu).
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa Nuur ´alaad-Darb (770)
- Imechapishwa: 10/03/2018
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket