Swali: Ni ipi nasaha yako kwa mwanafunzi ambaye amesoma kwa miaka mingi na ananuia kurudi katika mji wake ambapo kumeenea mapote na watu wa Bid´ah wanaoenda kinyume na Ahl-us-Sunnah?
Jibu: Ukirudi katika mji wako na Allaah amekutunuku elimu na ukaijua haki eneza elimu huko na uwalinganie watu katika dini ya Allaah. Allaah (Jalla wa ´Aala) amesema:
وَلِيُنذِرُوا قَوْمَهُمْ إِذَا رَجَعُوا إِلَيْهِمْ لَعَلَّهُمْ يَحْذَرُونَ
“… na ili waonye watu wao watakaporejea kwao ili wapate kutahadhari.” (09:122)
Ni wajibu kwako kufanya hivi. Simama kwa kutengeneza, kulingania katika dini ya Allaah na ueneze elimu ya Kishari´ah.
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Duruus-ul-Haram http://www.alfawzan.af.org.sa/node/13398
- Imechapishwa: 26/04/2018
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)