Swali: Ni ipi tofauti kati ya dufu na ngoma?

Jibu: Ngoma inajulikana. Baadhi ya wanazuoni wamesema kuwa ni sawa na ngoma. Hata hivyo dufu ndilo linaloruhusiwa na kilicho zaidi ya hilo hakiruhusiwi. Dufu linaruhusiwa kwa wanawake, nalo ni chombo cha pande moja kinachotengenezwa kwa ngozi au kitu kama hicho. Hakina pete za chuma wala vipande vya chuma vinavyotoa sauti. Dufu hupigwa na wanawake. Ama ngoma, kuna Hadiyth inayokataza. Vivyo hivyo ala nyingine zote za muziki. Vyote ni vitu vilivyoharamishwa.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/1196/الفرق-بين-الدف-والطنبور
  • Imechapishwa: 07/02/2026