Swali: Je, inafaa kufanya Tawassul kwa wafu? Ni ipi hukumu ya anayefanya Tawassul kwa wafu? Ni ipi Tawassul inayokubalika katika Shari´ah?
Jibu: Kufanya Tawassul kwa wafu katika yale wasiyoyaweza… na wao hakuna chochote wanachokiweza. Ni Bid´ah pale ambapo haijafikia katika kiwango cha imani. Tawassul inayokubalika kwa mujibu wa Shari´ah ni ku-Tawassul kwa majina na sifa Zake. Allaah (Ta´ala) amesema:
وَلِلّهِ الأَسْمَاء الْحُسْنَى فَادْعُوهُ بِهَا
”Allaah ana majina mazuri mno; hivyo basi muombeni kwayo.”[1]
Pia inafaa kufanya Tawassul kwa mtu aliye hai katika yale anayoyaweza. Yule bwana kipof ambaye alikuja kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kusema: ”Ee Muhammad! Mimi natawasali kwa du´aa yako mbele ya Mola wangu.” Mtume hapa alikuwa hai na muweza wa kumwombea. Pia inafaa kufanya Tawassul kwa matendo mema, kama ilivyo katika kile kisa cha watu wa pangoni.
[1] 07:180
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 26
- Imechapishwa: 22/07/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket