Swalah ya mkusanyiko kwa anayesukumwa kwenye kiti cha magurudumu II

Swali 217: Mlemavu aliye juu ya kiti cha magurudumu analazimika kuajiri mtu wa kumsukuma kwa ajili ya swalah ya mkusanyiko?

Jibu: Hapana, si lazima kwake. Ni mwenye kupewa udhuru. Na akifanya hivo, basi Allaah atamlipa kheri.

218 – Je, haisemwi: “Kitu ambacho wajibu haukamiliki isipokuwa kwacho, basi nacho ni wajibu”?

Jibu: Huyu ni mlemavu. Anajikokota kwa kutambaa na anayejikokota kwa kutambaa si wajibu kuhudhuria [… wangeliiendea ijapo kwa kutambaa].

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Masaa-il-ul-Imaam Ibn Baaz, uk. 90-91
  • Imechapishwa: 02/05/2025
  • Mkusanyaji: Shaykh Abiy Muhammad ´Abdullaah bin Maaniy´