Swali: Mtu akipitwa na swalah kutokana na udhuru. Je, inafaa kuichelewesha baada ya kuondoka udhuru?
Jibu: Haijuzu kwako kuchelewesha swalah nje ya wakati wake ukiondoka udhuru. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Yule mwenye kupitikiwa na usingizi au akaisahau swalah, basi aiswali pale atapoikumbuka. Haina kafara nyingine isipokuwa hiyo.”[1]
Amefanya kuwa inakidhiwa pale tu inapokumbukwa. Ukichelewesha zaidi, unapata dhambi.
[1] al-Bukhaariy (597) na Muslim (684).
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (12/224)
- Imechapishwa: 10/04/2026
Swali: Mtu akipitwa na swalah kutokana na udhuru. Je, inafaa kuichelewesha baada ya kuondoka udhuru?
Jibu: Haijuzu kwako kuchelewesha swalah nje ya wakati wake ukiondoka udhuru. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Yule mwenye kupitikiwa na usingizi au akaisahau swalah, basi aiswali pale atapoikumbuka. Haina kafara nyingine isipokuwa hiyo.”[1]
Amefanya kuwa inakidhiwa pale tu inapokumbukwa. Ukichelewesha zaidi, unapata dhambi.
[1] al-Bukhaariy (597) na Muslim (684).
Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (12/224)
Imechapishwa: 10/04/2026
https://firqatunnajia.com/swalah-iliyompita-mtu-inaswaliwa-haraka-iwezekanavyo/