Swali: Niko katika Rak´ah ya kwanza ya Sunnah halafu kukakimiwa swalah. Je, niikate?
Jibu: Ikiwa unaweza kuikhafifisha na ukatoa Tasliym kabla imamu hajarukuu, fanya hivo. Lakini ikiwa imamu atarukuu kabla ya wewe kukamilisha swalah yako, ikate.
Swali: Nitole Tasliym upande wa kulia na wa kushoto endapo nitaikata?
Jibu: Hukuikamilisha. Tasliym inatolewa wakati wa kukamilisha:
“Ufunguzi wa swalah ni twahara. Uharamu wake ni Takbiyr na uhalali wake ni Tasliym.”[1]
[1] Abu Daawuud (618), at-Tirmidhiy (3), Ibn Maajah (275), ash-Shaafi´iy (1/34), Ibn Abiy Shaybah (1/208) na Ahmad (1006). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”Swahiyh Sunan Abiy Daawuud” (55).
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (6) http://alfawzan.af.org.sa/node/14379
- Imechapishwa: 26/11/2016
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket