Swali: Nimjibu vipi mtu ambaye ananiuliza kama mimi ni Salafiy?
Jibu: Ni utukufu. Sema kuwa wewe ni Salafiy kwa fakhari. Jibu rahisi. Ni nini maana ya Salafiy? Salafiy maana yake ni kwamba mimi nawafuata wale waliotangulia katika Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam), Maswahabah wake watukufu na makhaliyfah wake waongofu ambao Allaah (Jalla wa ´Alaa) amesema juu yao:
وَالسَّابِقُونَ الْأَوَّلُونَ مِنَ الْمُهَاجِرِينَ وَالْأَنصَارِ وَالَّذِينَ اتَّبَعُوهُم بِإِحْسَانٍ رَّضِيَ اللَّـهُ عَنْهُمْ وَرَضُوا عَنْهُ
“Wale waliotangulia wa mwanzo [katika Uislamu] miongoni mwa Muhaajiruun na Answaar na wale waliowafuata kwa wema, Allaah ameridhika nao nao wameridhika Naye.”[1]
Lakini usifikirie kuwa kila mtu atakuwa radhi nawe. Kinyanyue kichwa chako na sema kwamba wewe ni Salafiy. Hakuna neno.
[1] 09:100
- Muhusika: Shaykh Swaalih bin ´Abdil-´Aziyz Aalush-Shaykh
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://www.youtube.com/watch?v=Bgo0kcWJihY&feature=youtu.be
- Imechapishwa: 22/05/2019
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)