Jipime maarifa yako kuhusu wudhuu´ na swalah
Chemsha Bongo ya twahara na swalah 02
15:00
Vipi wudhuu wangu ikiwa nimeosha baadhi au viungo vyote mara mojamoja?
- Wudhuu´ hausihi
- Wudhuu´ hana na lazima atawadhe tena
- Wudhuu´ umesihi
Je, inahabika swalah ya mwenye kusoma Qur-aan kwa sauti ya juu kwenye Dhuhr na Aswr?
- Ndio
- Hapana, haiharibiki amekhalifu Sunnah tu
- Lazima arudi swalah yake
Je, vipi swalah ya mtu ambaye ana paketi ya sigara mfukoni?
- Haisihi na arudi kuswali
- Swalah yake inasihi
- Hana wudhuu´ wala swalah
Je, inafaa kuswali na viatu?
- Hapana, hayo ni matendo ya manaswara makanisani
- Ndio, bali kufanya hivo ni Sunnah
- Ndio, kwa sharti viatu viwe viapya
Ni kipi kinachotangulia kupanguswa katika Tayammum kati ya uso na viganga vya mikono?
- Uso
- Mguu
- Viganja vya mikono
Je, inafaa kwa mtu kutawadha kwa chai au juisi ikiwa hana maji?
- Hapana, haifai na wudhuu´ hausihi
- Ndio, inafaa
- Anaweza ikiwa chai au juisi ni safi
Ikiwa mgonjwa ana udhuru wa kutoswali ikiwa amelazwa hospitali na mavazi yake saa zote ni machafu?
- Ndio, anao udhuru
- Hapana, ataswali vovyote vile kutegemea hali yake
- Ataswali baada ya kupona
Je, inasihi swalah ya ambaye amekusudia kusoma al-Faatihah peke yake?
- Hapana, haisihi
- Ndio, inasihi
- Inategemea ni faradhi au Sunnah
Je, anatakiwa kurudia wudhuu mtu anayepatwa na wasiwasi wa twahara yake mara kwa mara?
- Hapana, hatakiwi kurudia
- Ndio, anatakiwa
- Atakiwi ikiwa amehisi maji mwilini
Je, ni lazima kuosha kila kiungo mara tatu wakati wa wudhuu?
- Hapana, si lazima
- Ndio, ni lazima
- Ni lazima kwa uso tu
Je, kicheko ndani ya swalah kinaharibu swalah?
- Tabasamu haiharibu swalah
- Ndio, kichezo kikubwa kinaharibu
- Inafaa kucheka ndani ya swalah hapana vibaya
Je, ni ipi hukumu ya kuweka nia ya swalah kwa kutamka kwa sauti?
- Ni Sunnah vinginevyo mtu hana swalah
- Si lazima kuweka nia kwa ajili ya swalah
- Kuweka nia kwa kutamka kwa sauti ni Bid´ah
Je, kipi sahihi katika haya?
- Kuwa na akili ni moja katika nguzo za swalah
- Kuwa na akili ni moja katika sharti za swalah
- Kuwa na akili ni moja katika Sunnah za swalah
Je, inafaa imamu wa msikiti kukusanya swalah wakati wa mvua?
- Hapana, haifai
- Ndio, ni Sunnah
- Inategemea na nchi mtu anaishi
Ni ipi hukumu ya kukusudia kutosema (Rabbiy Ighfirliy) katika Rukuu?
- Hapana, si lazima na swalah ni sahihi
- Ndio, ni lazima na hivyo hana swalah
- Inategemea hali ya mtu
Ni kipi katika haya ni nguzo mojawapo ya swalah?
- Kunyanyua mikono wakati wa Takbiyrat-ul-Ihraam
- Kuelekea Qiblah
- Kusoma al-Faatihah
Je, swalah ya mtu aliyesahau kuketi kati ya sujuud mbili imeharibika?
- Hapana, haijaharibika
- Ndio, imeharibika
- Inategemea ni swalah ya faradhi au ya sunnah
Je, swalah ya mtu inabatilika akiacha kusoma al-Faatihah kwa kusahau?
- Hapana, haibatiliki
- Ndio, inabatilika na lazima aswali tena
- Inategemea ikiwa ni swalah ya faradhi au sunnah
Je, anakufuru mwenye kuacha kuswali makusudi?
- Hapana, hakufuru
- Ndio, sahihi ni kwamba anakufuru
- Hakufuru kama ni muislamu safi
Ni kipi katika haya ni sahihi?
- Swalah ya aliyepiga Siwaak ni bora zaidi kuliko ya ambaye hakupiga
- Zote zinalingana
- Swalah ya aliyepiga Siwaak ni bora zaidi ikiwa ni ya faradhi tu na si ya Sunnah
Je, inafaa kwa mtu kuswali huku amevaa nguo chafu lakini si najisi?
- Ndio, inafaa
- Hapana, haifai
- Inafaa tu ikiwa hana nguo nyingine
Ni ipi hukumu ya kuswali huku unahisi haja kubwa au ndogo?
- Ndio, ni haramu na swalah haisihi
- Inategemea muda wa swalah
- Ni jambo linalochukiza na swalah inafaa