Jipime maarifa yako kuhusu twahara na swalah

Chemsha Bongo ya twahara na swalah 12

15:00

Ni nani ana haki zaidi ya kumswalia maiti?

Mtu anatumia mkono gani wakati wa kupenga?

Vipi twahara ya mwanamke aliyepaka rangi ya kucha inayozuia maji kufika kwenye kucha?

Je, inafaa kutumia maji ya zamzam kwa ajili ya kutamba?

Ni Suurah ipi inayosema swalah inamzuia mtu kutokana na machafu na maovu?

Ni usingizi upi unachengua wudhuu?

Ni msafiri wa siku ngapi anazingatiwa na kuruhusiwa kufupisha swalah?

Sunnah na bora mtu afanye Adhkaar kwa mkono wa kuume au kushoto au yote miwili?

Je, inafaa mara kwa mara kukusanya kati ya Maghrib na Ishaa mchana unapokuwa mrefu na kesho mtu ataamkia kazini au shuleni?

Je, inafaa kumswalia maiti ambaye alikuwa haswali kabisa?

Je, inafaa kwa msafiri kukusanya kati ya Ijumaa na Aswr?

Ni lazima kuelekea Qiblah wakati wa kutawadha?

Swalah ya faradhi inasihi juu ya kipando kwa kukaa?

Mtu aliyekosa Dhuhr na umefika wakati wa Aswr, anaanza na swalah gani?

Ni nyama ya mnyama upi inachengua wudhuu katika hizi?

Ni ipi hukumu ya mazowea watu kupeana mkono (kusalimiana) baada ya kumaliza swalah ya mkusanyiko msikitini?

Kabla ya kuanza swalah unatakiwa kuhakikisha umeondosha najisi sehemu tatu. Ni zipi?

Ni ipi hukumu ya kutumia maji ya bwawa au mto ambayo mtu hajui usafi wake?

Je, inafaa kushika utupu kwa mkono wa kulia?

Ni ipi hukumu ya kuswali na nguo yangu iliyopatwa na mkojo wa kondoo au mbuzi?

Ni ipi hukumu ya kusoma Basmalah kwa sauti mwanzoni mwa Suurah ndani ya swalah?

Ni ipi hukumu ya kupitisha maji kati ya vidole vya miguu wakati wa kutawadha?